Mwanachama wa al-Shabaab akosoa uongozi wa kikundi

Aprili 01, 2012

  • + Toa maoni sasa
  • Chapisha
  • Panga upya Punguza Ongeza

Mwanachama wa al-Shabaab Hasan Dahir Aweys amekosoa kikundi kwa mauaji ya bure bure ya raia na kwa kushirikiana kwake na al-Qaeda, Shirika la Habari la Taifa la Somalia liliripoti hapo Jumapili (tarehe 1 April).

Aweys, kiongozi wa zamani wa kikundi chenye itikadi kali cha Somalia Hizbul Islam, alikiambia kikundi cha washirika wake wa karibu huko Elasha Biyana siku ya Jumamosi kuwa ushirika wa al-Shabaab na al-Qaeda usingekubalika na aliwashutumu wanamgambo kwa kumwaga damu isiyo na hatia bila sababu yoyote.

Alisema wakazi wanawaogopa al-Shabaab kwa sababu ya ukorofi wa vurugu zake, ambazo zinaivunjia al-Shabaab hadhi ya malengo yake, na kuongeza kuwa kikundi cha wanamgambo kingepaswa kuchukua tahadhari ya kutowaingiza raia katika mapigano.

Mwezi huu, kiongozi wa al-Shabaab Omar Hammami, anayejulikana pia kama Abu Mansoor al-Amriki, alieleza kutokubaliana kwake na kikundi hiki katika video iliyotumwa mtandaoni akielezea hofu ya maisha yake.

Unaonaje kuhusu makala hii? (Jumla ya Kura 3)

Dislike_icon(0)

(Sera za kutoa Maoni) *Inaonesha Maeneo yanayohitaji

Habari Mpya kabisa

Katika Mwangaza

Jisajili

Kura

Je, unadhania kupigwa marufuku kwa hotuba ya chuki na Tanzania kutakomesha mashambulizi dhidi ya makanisa na misikiti?

Angalia matokeo

Nyenzo