Aprili 01, 2012
Somalia imeiondoa moja ya ngome za al-Shabaab iliyobakia karibu na Mogadishu Jumamosi (tarehe 31 Machi), baada ya mapigano ya siku moja kati ya wapiganaji na wanajeshi wa Serikali ya Mpito ya Shirikisho (TFG) wakisaidiwa na vikosi vya Umoja wa Afrika, wakazi wenyeji waliiambia AFP.
Familia za Somalia walitumia nafasi ya utulivu katika mapigano kuondoka katika wilaya ya Daynile nje ya Mogadishu, ambako mapigano ya Ijumaa yaliua takribani watu kumi, kwa mujibu wa Mtandao wa Habari wa Shabelle wa Somalia. Daynile inasaidia kufika katika ushoroba wa Afgoye, barabara inayounganisha Mogadishu na mkoa wa Lower Shabelle.
Katika wiki chache zilizopita, maelfu ya wakazi wameondolewa Daynile kabla ya shambulio liliotarajiwa kufanywa na vikosi vya AMISOM na Somalia.
Kamanda wa jeshi la TFG Abdullahi Yare, ambaye yuko katika kituo cha ukaguzi cha Afgoye, alisema shughuli zimerejea katika hali ya kawaida katika njia ya Afgoye baada ya kuwa imefungwa kutokana na mapigano, Shabelle iliripoti. Wakazi waliithibitishia AFP kwamba barabara ilifunguliwa tena.
Misheni ya Umoja wa Afrika huko Somalia ilisema siku ya Ijumaa kwamba vikosi vya muungano vimeiteka wilaya kutoka kwa al-Shabaab.
"Operesheni ya kijeshi huko Daynile ilikuwa ya mafanikio na mabaki ya washirika wa al-Qaeda waliondolewa,” kamanda wa jeshi la TFG Abdikarim Yusuf Dhego-Badan aliwaambia waandishi wa habari. “Vikosi vyetu sasa viko karibu katika kila sehemu ya wilaya na hali ni ya utulivu.”
Al-Shabaab nao pia walidai kushinda katika mapambano.
Kikundi cha msaada wa matibabu cha Madaktari Wasio na Mipaka (MSF) kilisema hospitali ya Daynile ilishambuliwa siku ya Ijumaa, na kutoa wito kwa pande zinazopigana kuheshimu hali ya hospitali kutokuwa upande wowote katika vita.
"Wodi ya dharura na sehemu moja ya chumba cha upasuaji katika hospitali hiyo, ambako MSF wamekuwa wakifanya kazi tangu 2006, vilishambuliwa na kusababisha uharibifu mkubwa,” kundi hilo lilisema katika kauli yake.
Hakuna madaktari au wagonjwa waliojeruhiwa. Wagonjwa wote 19 na wafanyakazi 48 kwa sasa wamejificha ndani ya wodi wakijikinga na mapigano, MSF walisema.
Polisi nchini Tanzania walimkamata mbunge wa Iringa Mjini, Peter Msingwa, na wafanyabiashara 60 k...
Mahakama moja ya Bosaso iliwatia hatiani na kuwapiga faini Wairani 78 siku ya Jumapili (tarehe 19...
Polisi nchini Tanzania waliwakamata watuhumiwa 15 kuhusiana na kulichoma Kanisa la Bethania kweny...
Mkuu wa Polisi wa Kenya, David Kimaiyo, ameondoa nafasi za afisa polisi wa jimbo, afisa wa upelel...
Watu wenye silaha waliwaua watu wawili na kuwajeruhi wengine wanne katika mashambulizi tofauti kw...
Mkutano wa kuzungumzia uwezekano wa uchimbaji mafuta na gesi, uwekezaji, usalama na miundombinu n...
Wizara ya Masuala ya Wanawake na Familia ya Puntland ilianza mafunzo ya siku nane hapo Juampili (...
Zaidi ya Wasomali milioni 1 hawatakuwa na "usalama wa chakula" hadi mwezi wa Septemba, Mtandao wa...
Ujumbe kutoka Jumuiya ya Maendeleo ya Pembe ya Afrika (IGAD) uliwatembelea maafisa mjini Mogadish...
Mshukiwa wa ugaidi na mke wake walipigwa risasi na kufa na maafisa sita wa polisi walijeruhiwa wa...
(Sera za kutoa Maoni) *Inaonesha Maeneo yanayohitaji