Makombora mawili yashambulia mwambao wa Kenya

Aprili 01, 2012

  • 2 Maoni
  • Chapisha
  • Panga upya Punguza Ongeza

Si chini ya mtu mmoja aliuawa na 18 kujeruhiwa katika mashambulio mawili yaliyolenga mkusanyiko katika kanisa huko Mtwapa na katika mgahawa huko Mombasa Jumamosi (tarehe 31 Machi), kwa mujibu wa Shirika la Msalaba Mwekundu la Kenya na maofisa wa jeshi la polisi.

Polisi walisema kifaa cha mlipuko, kinachowezekana kuwa ni kombora, kilirushwa katika mkusanyiko huko Mtwapa muda wa kama saa 2 usiku. “Watu kumi na sita walijeruhiwa, wawili walijeruhiwa vibaya, na mmoja alikufa,” Nelly Muluka, msemaji wa Shirika la Msalaba Mwekundu aliimbia AFP, akiongezea kuwa majeruhi wamebakia hospitalini.

Mkuu wa polisi wa jimbo la Pwani Aggrey Adoli aliiambia AFP kuwa kombora la pili lilirushwa kwenye mgahawa huko Mombasa” dakika chache baadaye, lilijeruhi watu watatu, akiwemo ofisa mmoja wa polisi. Mmoja wa walioathirika amebakia hospitali, Muluka alisema. Wakazi wa eneo hilo walisema mgahawa huo unajulikana kwa kuhudumia milo ya nyama ya nguruwe.

Hakuna yeyote aliyedai mara moja kuhusika na mashambulio ya Jumamosi na mamlaka husika hazijasema lolote kuhusu nani anaweza kuhusika na mashambulio hayo.

Unaonaje kuhusu makala hii? (Jumla ya Kura 2)

Dislike_icon(1)

(Sera za kutoa Maoni) *Inaonesha Maeneo yanayohitaji

Maoni ya msomaji

  • Beth Kagunya
    April 2, 2012 @ 05:06:05AM

    Hata kanisani watu wachunguzwe ili kuepuka maafa.

  • Mohammed Noor
    April 2, 2012 @ 12:27:41AM

    Jamani, hiyo inaonesha jeshi letu la Kenya halifanyi kitu, vinginevyo wangepata somo kutokana na milipuko iliyotangulia ya Garisaa na Nairobi. ANEYEPIGWA MARA MOJA, HUONA HAYA MARA YA PILI. Mohammed Noor mkazi wa Isiolo.

Habari Mpya kabisa

Katika Mwangaza

Jisajili

Kura

Je, unadhania kupigwa marufuku kwa hotuba ya chuki na Tanzania kutakomesha mashambulizi dhidi ya makanisa na misikiti?

Angalia matokeo

Nyenzo