Guelleh azindua ligi ya Mpira wa Miguu Jibuti

Machi 28, 2012

  • + Toa maoni sasa
  • Chapisha
  • Panga upya Punguza Ongeza

Rais wa Jibuti Ismail Guelleh alizindua ligi ya mpira wa miguu ya taifa huko Dikhil siku ya Jumatatu (tarehe 26 Machi), itakayochukua mikoa mitano ya nchi, gazeti la La Nation la Jibuti liliripoti.

Rais alitumia uwanja wa michezo wa Manispaa huko Dikhil kupokea bendera na mwenge wa umoja kutoka katika mikono ya vijana wawili. Viongozi wa serikali na mamia ya vijana walishangilia kutoka kila upande, gazeti liliripoti.

Hii ni mara ya kwanza kwa ligi ya mpira wa miguu ya mkoa kuundwa nchini Jibuti. Katibu Mkuu wa nchi kwa ajili ya Vijana na Michezo Djama Elmi Okieh alisema michezo inapaswa kufanyika nchi nzima, na sio jijini tu.

Ushiriki wa taifa katika michezo hautakuwa katika mpira wa miguu tu, alisema Okieh. "Kutakuwa na mashindano ya mabingwa wa mpira wa mikono, mpira wa kikapu, mpira wa wavu n.k., na katika kila wilaya ya Jibuti, kutakuwa na mashindano ya ubingwa wa kila fani," alisema waziri.

Unaonaje kuhusu makala hii? (Jumla ya Kura 0)

Dislike_icon(0)

(Sera za kutoa Maoni) *Inaonesha Maeneo yanayohitaji

Habari Mpya kabisa

Katika Mwangaza

Jisajili

Kura

Je, unadhania kupigwa marufuku kwa hotuba ya chuki na Tanzania kutakomesha mashambulizi dhidi ya makanisa na misikiti?

Angalia matokeo