AMISOM yashutumu ‘kampeni za uoga’ za al-Shabaab

Machi 22, 2012

  • 3 Maoni
  • Chapisha
  • Panga upya Punguza Ongeza

Kamanda anayemaliza muda wake wa kikosi cha AMISOM Meja Jenerali Fred Mugisha ameshutumu mashambulio ya hivi karibuni ya al-Shabaab jiji la Mogadishu na kuwatuliza Wasomali kuwa usalama unaboreshwa.

“Mashambulio haya ni sehemu ya kampeni zao za kujenga uoga na kuogofya watu,” alisema katika taarifa iliyotolewa Alhamisi (tarehe 22 Machi). “Wasomali wote ni lazima wasimame imara dhidi ya maadui hawa wa amani. Tunawahimiza kutuletea taarifa kuhusu mashambulio na milipuko inayoweza kutokea. Tutasimama nanyie kwa kuwa tunatafuta kujenga njia nzuri ya maisha."

Al-Shabaab wamewaonya raia kuepuka majengo ya serikali na vituo vya AMISOM , kwani bado yatabakia kuwa sehemu zinazolengwa kwa mashambulio, Mtandao wa Habari wa Shabelle wa Somalia uliripoti.

“Tunatuma ujumbe wa onyo kwa wasomali wote kutokuwa karibu na vituo vya jeshi la Serikali ya Mpito ya Shirikisho ya Somalia na vituo vya jeshi la AMISOM kuepuka kupoteza maisha kutokana na mashambulio ya kumwaga damu,” alisema msemaji wa al-Shabaab Shekhe Ali Mohamud Rage.

Mugisha alisema wanamgambo walioshirika na al-Qaeda hawahusiki na ustawi wa raia. “Iwapo wangekuwa wanatafuta kuboresha hali ya watu, wasinge washambulia raia wasio na silaha,” alisema.

Vikosi vya Umoja wa Afrika na vya Somalia vimekuwa vikifanya kazi kwa kushirikiana na raia kuzuia hadi asilimia 70 ya zana za mlipuko zilizochimbiwa katika mji huu, kwa mujibu wa AMISOM.

Unaonaje kuhusu makala hii? (Jumla ya Kura 3)

Dislike_icon(1)

(Sera za kutoa Maoni) *Inaonesha Maeneo yanayohitaji

Maoni ya msomaji

  • Fu'aad Axmed
    March 24, 2012 @ 11:38:45PM

    Al-Shabaab wamekuwa tishio kubwa sana kwa kutilia maana ni kuwa wanafuata itikadi kali za al-Qaeda. Suluhisho pekee kwa hali ya Somalia ni kuongeza operesheni za kijeshi ili kuwatoa al-Shabaab au njia nyingine ni kuwa na mazungumzo ya amani pamoja na magaidi. Mchakato wa amani unaweza kuchukua muda mrefu lakini hatimaye kutakuwa na amani nchini Somalia.

  • isaac koech
    March 23, 2012 @ 05:20:55AM

    Al-Shabaab hawawezi kukaribia kuwashinda AMISOM.

  • Surayya
    March 22, 2012 @ 10:51:46PM

    Kundi la Alshabab linafanya majuhudi kwa kuingiza vijana kwa shida na kuwapatia masilaha na kuwangiza kwa kundi lao bado waki wadogo kwa umri na wakati zingine kwa nguvu kwa vile tunajua mambo ndani ya Somalia hayazoleki, na kwa kwa bahati mbaya kuna maeneo mengi na vijiji kwa mkono ya Alshabab wakiendelea uhalifu na dhulma zao dhidi ya watu maskini na wale wasiopata hata kitu ya kukula.

Habari Mpya kabisa

Katika Mwangaza

Jisajili

Kura

Je, unadhania kupigwa marufuku kwa hotuba ya chuki na Tanzania kutakomesha mashambulizi dhidi ya makanisa na misikiti?

Angalia matokeo