Kenya yapanga tarehe ya uchaguzi kuwa tarehe 4 Machi 2013

Machi 18, 2012

  • 1 Maoni
  • Chapisha
  • Panga upya Punguza Ongeza

Siku ya Jumamosi (tarehe 17 Machi) Kenya imetangaza kwamba uchaguzi mkuu ujao utafanyika tarehe 4 Machi, 2013, ikimaliza wiki ya mabishano makali baina ya wanasiasa wapinzani, AFP iliripoti.

"Tunafuata uamuzi wa mahakama ya katiba…ambao unatutaka kufanya uchaguzi siku 60 kuanzia siku muda wa bunge utakapokwisha,”alisema Ahmed Issack Hassan, mwenyekiti wa Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka ya Kenya (IEBC).

Hata hivyo, mahakama pia ilisema uchaguzi ungeweza kufanyika mapema kama kungekuwa na makubaliano ya maandishi kati ya Raisi Mwai Kibaki na Waziri Mkuu Raila Odinga kuivunja serikali ya mseto.

IEBC ilisema haijapokea uamuzi kuhusu jambo hilo baada ya kukutana na viongozi hao wawili, na hivyo, iliamua kuchukua hatua ya kupanga tarehe.

"Imekuwa dhahiri kwetu kwamba hawakusudii kuvunja mseto….Kuna kutokubaliana miongoni mwao kuhusu ni lini kura inapaswa kupigwa,” Hassan alisema. “Ndiyo maana tulijiamulia wenyewe kupanga tarehe.”

Unaonaje kuhusu makala hii? (Jumla ya Kura 5)

Dislike_icon(0)

(Sera za kutoa Maoni) *Inaonesha Maeneo yanayohitaji

Maoni ya msomaji

  • Edson Gwako
    March 19, 2012 @ 02:46:57AM

    WOTE MHESHIMIWA WAZIRI MKUU NA MTUKUFU RAISI NI WASHINDANI WA KISIASA. RAILA NA ODM WANATAKA WAPATE URAISI NA KIBAKI ANATAKA KUHAKIKISHA PNU KINAPATA URAISI. IKIWA WATATEGEMEA TAREHE YA UCHAGUZI, BADO KUTATOKEA MABABAIKO. IEBC LAZIMA IONGOZE NJIA, LAKINI NJIA INGEKUWA IKUBALIANE NA KATIBA MPYA YA KENYA NA IONEKANE NI HAKI NA WAKENYA WALIO WENGI.

Habari Mpya kabisa

Katika Mwangaza

Jisajili

Kura

Je, unadhania kupigwa marufuku kwa hotuba ya chuki na Tanzania kutakomesha mashambulizi dhidi ya makanisa na misikiti?

Angalia matokeo