Baraza la Mawaziri la Somalia limefanya Mkutano wa dharura baada ya ulipuaji wa bomu Villa Somalia

Machi 16, 2012

  • 1 Maoni
  • Chapisha
  • Panga upya Punguza Ongeza

Baraza la Mawaziri la Somalia lilifanya kikao cha dharura Alhamisi (tarehe 15 Machi) baada ya shambulio la bomu la kujitoa muhanga lililoua watu watano katika makazi ya rais, Mtandao wa Habari wa Shabelle wa Somalia uliripoti.

Mkutano huo ambao haukuruhusu waandishi wa habari au umma kuingia uliongozwa na Waziri Mkuu Abdiweli Mohamed Ali, baada ya hapo msemaji wa serikali Abdirahman Omar Osman “Yarisow” alisoma taarifa akibainisha mlipuaji kuwa ni Omar Garweyne, Shirika la habari liliripoti.

Mmoja wa [wafanyakazi] kutoka ofisi ya rais… alimsaidia mlipuaji kufika katika eneo la kasri,” AFP ilimnukuu Yarisow wakati akisema. Mlipuaji alipita vituo vitatu vya ukaguzi, baada ya hapo alilipua fulana yake iliyokuwa na bomu, akijiua mwenyewe na watu wengine watano akiwemo mshirika wake, AFP iliripoti.

Al-Shabaab walidai kuhusika na shambulio hilo na kutoa wito kwa wasomali “kushiriki katika vita dhidi ya makafiri na Serikali iliyoasi dini” msemaji wa al-Shabaab Sheikh Ali Mohamud Gare alisema Jumatano jioni, kwa mujibu wa AFP.

Al-Shabaab wameamua kutumia mbinu za wapiganaji wa msituni baada ya kuondolewa katika ngome zake huko Mogadishu mwezi Agosti.

Unaonaje kuhusu makala hii? (Jumla ya Kura 1)

Dislike_icon(0)

(Sera za kutoa Maoni) *Inaonesha Maeneo yanayohitaji

Maoni ya msomaji

  • hisherm
    March 16, 2012 @ 09:28:32PM

    Somalia ni nchi iliyo na mchanganyiko wa Waafrika, Waislamu na Waarabu, kwa hivyo, utambulisho huu lazima udumishwe na uingiliaji kati wowote, uwe wa kikanda au wa kimataifa, lazima uzingatie muundo huo.

Habari Mpya kabisa

Katika Mwangaza

Jisajili

Kura

Je, unadhania kupigwa marufuku kwa hotuba ya chuki na Tanzania kutakomesha mashambulizi dhidi ya makanisa na misikiti?

Angalia matokeo