Vikosi vya Somalia, Ethiopia vyapambana na al-Shabaab huko Yurkut

Machi 11, 2012

  • + Toa maoni sasa
  • Chapisha
  • Panga upya Punguza Ongeza

Mapambano kati ya vikosi vya serikali ya Somalia vikisaidiwa na vikosi vya Ethiopia na wapiganaji wa al-Shabaab karibu na kijiji cha Yurkut cha Somalia Jumamosi (tarehe 10 Machi) yameua wapiganaji wengi wa pande zote, AFP iliripoti.

Afisa anayeiunga mkono serikali Kalif Adan alisema kwamba al-Shabaab waliivamia Yurkut Jumamosi asubuhi. "Wengi wao waliuawa katika mapigano makali. Mapigano sasa yamekwisha na al-Shabaab wamepigwa sana,” aliiambia AFP.

Kamanda wa al-Shabaab Sheikh Mohammad Abu Fatma pia alidai kushinda. “Wapiganaji wa mujahidina waliongoza uvamizi wao muhimu sana wa kijeshi dhidi ya maeneo ya adui huko Yurkut,” alisema.

Vyanzo vya jeshi katika makambi yote vilitoa idadi ya vifo inayotofautiana, lakini vilisisitiza ukali wa mapambano ya saa tatu, kwa mujibu wa AFP.

Yurkut ni sehemu muhimu barabarani inayounganisha mpaka wa Somalia na Ethiopia na Baidoa, iliyokuwa ngome ya al-Shabaab kusini mwa Somalia ambayo vikosi vya Ethiopia na Somalia viliiteka mwezi uliopita.

Unaonaje kuhusu makala hii? (Jumla ya Kura 0)

Dislike_icon(0)

(Sera za kutoa Maoni) *Inaonesha Maeneo yanayohitaji

Habari Mpya kabisa

Katika Mwangaza

Jisajili

Kura

Je, unadhania kupigwa marufuku kwa hotuba ya chuki na Tanzania kutakomesha mashambulizi dhidi ya makanisa na misikiti?

Angalia matokeo