Machi 08, 2012
Ujumbe wa Ulaya uliwasili Puntland Jumatano (tarehe 7 Machi) kutathmini juhudi dhidi ya uharamia katika mkoa huo, mtandao wa Habari wa Shabelle wa Somalia uliripoti.
Wawakilishi thelathini na watatu kutoka Uingereza, Norwe, Denmaki na Uholanzi walitembelea Garowe kuhakiki miradi dhidi ya uharamia inayogharimu mamilioni ya dola inayofadhiliwa na Ulaya, kwa mujibu wa Mkurugenzi anayekabili uharamia wa Puntland Abdirizak Mohamed Ducaysane.
Wakati huohuo, Umoja wa nchi za Ulaya uliahidi kuongeza ugharimiaji kwa Misheni ya Umoja wa Afrika nchini Somalia kwa dola milioni 132, pamoja na kuongeza uwepo wa jeshi lake katika maeneo maji ya Pembe za Afrika. Gazeti la Daily Nation la Kenya liliripoti Jumatano. Tangazo hili lilikuja kufuatia mkutano uliofanyika Brussels kati ya Waziri Mkuu wa Kenya Raila Odinga na rais wa Baraza la Ulaya Herman Van Rompuy.
Umoja wa Ulaya utaongeza operesheni za jeshi lake la majini katika Pembe ya Afrika hadi 2014, ukipeleka ujumbe wa kusimamia migogoro ya kiraia kujenga uwezo wa mambo ya bahari katika mkoa huo.
“Ni tumaini langu kuwa kwa kuunganisha nguvu tutaweza kuchangia kuongeza usalama nchini Somalia na kurejesha amani na utulivu katika nchi hii,” Van Rompuy alisema. Rais wa Ulaya pia aliishukuru Kenya kwa kuchangia maasikari kwa AMISOM.
Odinga, ambaye aliomba Ulaya na nchi nyingine kuendelea kuwajibika katika kuimarisha Somalia, alisema kuna “mwanga mwishoni mwa shimo refu la chini kwa chini la kutoka sehemu moja kwenda nyingine” kuhusiana na mgogoro wa Somalia, akiwataka kuwekeza kaskazini mwa Kenya pamoja na Somalia.
Polisi waliwakamata mamia ya watu wanaoshukiwa kuwa wapiganaji wa al-Shabaab katika wilaya za Hod...
Kongamano la siku tatu juu ya elimu lilifunguliwa mjini Mogadishu siku ya Jumanne (tarehe 18 Juni...
Wanajeshi wa serikali ya Somalia wakisaidiwa na wanajeshi wa Misheni wa Umoja wa Mataifa (AMISOM)...
Waziri wa Mambo ya Ndani na Uratibu wa Serikali ya Kitaifa, Joseph Ole Lenku, siku ya Jumatatu (t...
Moto kwenye soko kubwa la Garissa uliharibu zaidi ya maduka 100 usiku wa Jumatatu (tarehe 17 Juni...
Waziri wa Umoja wa Kitaifa wa Djibouti Zahra Youssouf Kayad alisaini mikataba ya miradi miwili ye...
Kamati ya bajeti ya Bunge ya Kenya imekataa pendekezo la kununua ofisi mpya kwa aliyekuwa Rais Mw...
Moto ulifanya uharibifu mkubwa katika mji wa Balbala huko Djibouti siku ya Jumapili (tarehe 16 Ju...
Picha ambazo al-Shabaab ilizituma siku za Jumapili (tarehe 16 Juni) kwenye mtandao wa Twitter za ...
Polisi nchini Kenya walimuua mtuhumiwa wa ugaidi, Kassim Omolo Otemo, mjini Mombasa wakati uvamiz...
(Sera za kutoa Maoni) *Inaonesha Maeneo yanayohitaji
Maoni ya msomaji
Kutokana na shughuli za maharamia nchi nyingi zinaogopa kufanya biashara na nchi ambazo njia zake za baharini zipo karibu na Somalia. Hii ina maanisha kuna ukuaji wa uchumi mdogo kwa sababu pesa nyingi zitatumika kulipia pesa za kukombolea au kutumia vikosi vya kijeshi ili kuongoza bidhaa.
Nimevunjwa moyo sana na msaada wa fedha uliopewa Puntland na Somaliland kutoka Jumuiya ya Ulaya. Ningependa kuwashauri wasichukue fedha hizo kwa sababu hazikutolewa kwa nia njema lakini kwa kukidhi maslahi yao ya uchoyo. Wanataka kuchukua mafuta yaliyogunduliwa Somalia kwa msaada wa fedha badala yake.