Rais wa Tanzania asisitiza usawa wa jinsia

Machi 06, 2012

  • + Toa maoni sasa
  • Chapisha
  • Panga upya Punguza Ongeza

Rais wa Tanzania Jakaya Kikwete amesisitiza wajibu wa serikali katika usawa wa jinsia siku ya Jumapili (tarehe 4 Machi) kabla ya mkusanyiko wa kimataifa wa watu wanaopanda Mlima Kilimanjaro kubainisha suala la unyanyasaji dhidi ya wanawake, gazeti la The Citizen la Tanzania liliripoti.

"Hatutasita katika jitihada hizi; Niko tayari kufanya kazi na wenzangu katika nchi nyingine kusitawisha chanzo hicho cha unyanyasaji katika bara la Afrika," Kikwete aliwaambia wawakilishi takriban 90 kutoka katika nchi 36 za Afrika, akiongeza kwamba unyanyasaji wa kijinsia unazizuia jamii kuendelea.

Kikwete aliwapongeza viongozi wa wilaya kwa kuungana ili kukabiliana na unyanyasaji wa kijinsia na kurejea itifaki katika Mkataba wa Afrika kuhusu Haki za Binadamu na Haki za Watu kuhusu Haki za Wanawake barani Afrika, unaojulikana vizuri kama Itifaki ya Maputo (Maputo Protocol), ambayo nchi 46 za Umoja wa Afrika zilitia saini na 28 kati yake zilithibitisha rasmi.

"Leo itifaki hiyo inatumika kama nyenzo muhimu kwa ajili ya kuikumbusha serikali iwajibike katika wajibu tulioufanya," Kikwete alisema.

Unaonaje kuhusu makala hii? (Jumla ya Kura 0)

Dislike_icon(0)

(Sera za kutoa Maoni) *Inaonesha Maeneo yanayohitaji

Habari Mpya kabisa

Katika Mwangaza

Jisajili

Kura

Je, serikali za majimbo ya shirikisho ziundwe vipi nchini Somalia kufuatia utata wa Jubbaland?

Angalia matokeo