Machi 02, 2012
Serikali ya Kenya inazindua mpango wa shilingi bilioni 1.8 (Dola za Marekani milioni 22) kufufua tasnia dhaifu ya nguo, ambayo imepata shida kwa miaka ya hivi karibuni kutokana na kuenea kwa upatikanaji wa nguo zilizotumika (mitumba), gazeti la Business Daily Africa liliripoti Alhamisi (tarehe 1 Machi).
Fedha ambazo zinatoka katika mkopo wa Benki ya Dunia zitatumika kupanua uzalishaji wa pamba, kuvifanya vinu vya kuchambulia pamba kuwa vya kisasa na kupandisha hadhi tasnia ya nguo, ambayo kwa sasa kinafanya kazi kwa uwezo wa asilimia 30, gazeti liliripoti.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda Karanja Kibicho alisema wizara itazindua kempeni ya "Nunua Kenya, Jenga Kenya" ili kupandisha hadhi nguo zinazotengenezwa nchini. " Hii itakatisha tamaa kukua kwa haraka kwa tasnia ya mitumba [nguo zilizotumika], ambayo kimsingi ni kumwaga bidhaa nchini," alisema Kibicho katika uzinduzi wa taasisi ya nguo na ngozi huko Thika.
Mamlaka ya Ukusanyaji Kodi ya Kenya imepandisha takribani mara mbili ushuru wa forodha wa usafirishaji wa kontena mwezi Desemba, pia iko katika mchakato wa kupandisha mara mbili bei ya nguo zilizotumika (mitumba), kwa mujibu wa chama cha wafanyabiashara cha Gikomba.
Polisi waliwakamata mamia ya watu wanaoshukiwa kuwa wapiganaji wa al-Shabaab katika wilaya za Hod...
Kongamano la siku tatu juu ya elimu lilifunguliwa mjini Mogadishu siku ya Jumanne (tarehe 18 Juni...
Wanajeshi wa serikali ya Somalia wakisaidiwa na wanajeshi wa Misheni wa Umoja wa Mataifa (AMISOM)...
Waziri wa Mambo ya Ndani na Uratibu wa Serikali ya Kitaifa, Joseph Ole Lenku, siku ya Jumatatu (t...
Moto kwenye soko kubwa la Garissa uliharibu zaidi ya maduka 100 usiku wa Jumatatu (tarehe 17 Juni...
Waziri wa Umoja wa Kitaifa wa Djibouti Zahra Youssouf Kayad alisaini mikataba ya miradi miwili ye...
Kamati ya bajeti ya Bunge ya Kenya imekataa pendekezo la kununua ofisi mpya kwa aliyekuwa Rais Mw...
Moto ulifanya uharibifu mkubwa katika mji wa Balbala huko Djibouti siku ya Jumapili (tarehe 16 Ju...
Picha ambazo al-Shabaab ilizituma siku za Jumapili (tarehe 16 Juni) kwenye mtandao wa Twitter za ...
Polisi nchini Kenya walimuua mtuhumiwa wa ugaidi, Kassim Omolo Otemo, mjini Mombasa wakati uvamiz...
(Sera za kutoa Maoni) *Inaonesha Maeneo yanayohitaji
Maoni ya msomaji
Ukosefu wa ajira unaoikumba Kenya ni kutokana na kutupa nguo kongwe katika nchi. Tuamke na kukubali kufufua viwanda vyetu kama ambavyo Chuo Kikuu cha Moi kimefanya.