Watuhumiwa wa Al-Shabaab warejeshwa mahakama ya Lamu

Machi 02, 2012

  • + Toa maoni sasa
  • Chapisha
  • Panga upya Punguza Ongeza

Watuhumiwa tisa wa kikundi cha al-Shabaab waliokamatwa na polisi wa Kenya wiki iliyopita wanatarajia kufikishwa mahakamani Ijumaa (tarehe 2 Machi) kwa mashtaka ya ugaidi, gazeti la Nairobi Star la Kenya liliripoti.

Watuhumiwa walirudishwa Lamu Jumatano, baada ya kupata matibabu ya majeraha ya risasi katika Hospitali ya General Coast huko Mombasa. Walikamatwa Kiunga na kupelekwa Lamu kabla ya kulazwa hospitalini. Polisi wa kupambana na ugaidi waliwarudisha watuhumiwa Lamu chini ya ulinzi mkali, liliripoti gazeti.

Watuhumiwa wote tisa walikana kuwa wafuasi wa al-Shabaab, wakisema walisafiri kwenda Somalia mapema mwezi huu kusheherekea sikukuu ya Maulid. Mahakama ilikataa maelezo yao, liliripoti gazeti.

Unaonaje kuhusu makala hii? (Jumla ya Kura 0)

Dislike_icon(0)

(Sera za kutoa Maoni) *Inaonesha Maeneo yanayohitaji

Habari Mpya kabisa

Katika Mwangaza

Jisajili

Kura

Je, unadhania kupigwa marufuku kwa hotuba ya chuki na Tanzania kutakomesha mashambulizi dhidi ya makanisa na misikiti?

Angalia matokeo