Kenya, Ethiopia zaipongeza operesheni ya ulinzi huko Somalia

Machi 02, 2012

  • + Toa maoni sasa
  • Chapisha
  • Panga upya Punguza Ongeza

Rais wa Kenya Mwai Kibaki na Waziri mkuu wa Ethiopia Meles Zenawi wameeleza kuunga kwao mkono operesheni za kijeshi huko Somalia dhidi ya al-Shabaab baada ya mkutano wa Nairobi Alhamisi (tarehe 1 Machi).

"Viongozi hao wawili walishukuru kwamba operesheni inayoendelea ya Vikosi vya Ulinzi vya Kenya kwa pamoja na wenzao wa Ethiopia na Somalia kutokomeza vitisho vilivyowekwa na waasi wa al-Shabaab vinafikia mwisho,” waziri wa Mambo ya Nje wa Kenya Moses Wetangula alisema baada ya mkutano, kwa mujibu wa shirika la habari la Xinhua la China .

Viongozi hao wawili pia walikaribisha uamuzi wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kuongeza AMISOM kutoka 12,000 hadi takriban 18,000 watumishi wa namna moja. Ongezeko la vikosi, walisema, litawezesha usambazaji katika maeneo yaliyokombolewa ili kuwezesha kuanzishwa kwa mifumo ya kiutawala kutakakofanywa na Serikali ya Somalia, utoaji wa misaada ya kibinadamu, na kurejea kwa watu wasio na makazi na wakimbizi katika majumbani kwao.

Kibaki na Zenawi waliripotiwa kusisitiza kwamba wakati kanda na jumuiya ya kimataifa wakiisaidia Somalia, wananchi wa Somalia wanapaswa kuijenga upya nchi yao na viongozi wa Somalia lazima wasuluhishe tofauti zao kwa manufaa ya nchi yao.

Unaonaje kuhusu makala hii? (Jumla ya Kura 1)

Dislike_icon(0)

(Sera za kutoa Maoni) *Inaonesha Maeneo yanayohitaji

Habari Mpya kabisa

Katika Mwangaza

Jisajili

Kura

Je, serikali za majimbo ya shirikisho ziundwe vipi nchini Somalia kufuatia utata wa Jubbaland?

Angalia matokeo