Machi 02, 2012
Wapiganaji wa al-Shabaab walilenga shambulizi katika mji wa Somalia wa kusini-magharibimwa Garbaharey usiku kucha hapo Alhamisi (tarehe 1 Machi) na kuua maafisa waandamizi wawili wa kijeshi na kuwajeruhi wengine kadhaa, Shirika la Habari la BBC liliripoti.
Al-Shabaab walitumia zana nzito, ikiwa ni pamoja na maroketi na magari yenye bunduki, katika jaribio la kuuteka upya mji wa kimkakati, ambao ilikuwa imeushikilia mpaka mwaka jana. Garbaharey sasa unatumiwa na wanajeshi wa Ethiopia na wa Serikali ya Mpito ya Shirikisho ya Somalia (TFG) kama kambi ya kuwashambulia al-Shabaab.
Mapigano yaliendelea hadi Ijumaa asubuhi, lakini askari wa Somalia waliukamata mji huo. "Garbaharey bado uko katika udhibiti wetu," alisema mbunge wa eneo hilo Muhammad Sayyid Adan. "Tulipoteza watu wawili katika vita, na majeruhi hawako katika hali mbaya," alisema.
Wapiganaji watano wa al-Shabaab waliuliwa katika mapigano hayo, alisema Jamal Hassan Sarey, mkuu wa vikosi vya TFG huko Garbaharey, kwa mujibu wa Redio ya Somalia Radio Bar-kulan.
Baadhi ya wabunge wa Somalia wameitupilia mbali hoja ya kumtaka waziri mkuu na baraza lake la maw...
Wabunge wa upinzani walidai kwamba serikali ya Tanzania imekuwa ikibana uhuru wa kujieleza na kud...
Sampuli ya DNA iliyochukuliwa kwenye mswaki uliokuwemo kwenye begi lililokuwa na risasi lililopat...
Wakenya kumi na wasaba wameshtakiwa kwa kuvunja amani, kufanya ghasia na ukatili dhidi ya wanyama...
Al-Shabaab imedai kuhusika na urushwaji wa makombora kwenye kasri ya rais mjini Mogadishu siku ya...
Wanajeshi wa Uganda wa Kikosi Namba 9+ wanarudi nyumbani baada ya kukamilisha miezi 13 ya ziara y...
Kikosi cha polisi cha Kenya kitaanza uhakiki wa kina wa maofisa mwezi ujao, kikianza na kusaili w...
Ujambazi ulizuiwa katika ofisi za usalama za Wells Fargo huko Mombasa ulisababisha kifo cha watu ...
Rais wa Ghana John Dramani Mahama aliahidi msaada wa nchi yake katika kipindi cha ujenzi mpya wa ...
Polisi nchini Tanzania walimkamata mbunge wa Iringa Mjini, Peter Msingwa, na wafanyabiashara 60 k...
(Sera za kutoa Maoni) *Inaonesha Maeneo yanayohitaji