Watendaji wa mizigo kuongeza ufanisi

Februari 23, 2012

  • + Toa maoni sasa
  • Chapisha
  • Panga upya Punguza Ongeza

Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA) inashughulikia mpaka asilimia 40 ya makontena huko Dar es Salaam wakati Huduma za Kimataifa za Makontena Tanzania (TICTS) inafanya ukarabati ili kuboresha ufanisi, gazeti la Daily News la Tanzania liliripoti Alhamisi (tarehe 23 Februari).

"TICTS inakarabati kreni yake ya melini hadi ufukweni. [Kwa vile] kuna kazi ya ujenzi inaendelea, TPA imeingilia kati katika kuziba pengo,” alisema Emmanuel Mallya, mkuu wa Shirika la Wakala wa Meli Tanzania.

Wiki iliyopita, Mamlaka ya Usafiri wa Nchi Kavu na Baharini (SUMATRA) aliwapa TICTS na mawakala wa kupokea na kuhamisha mizigo miezi mitatu kuboresha ufanisi ili kuepusha kuchelewa kwa mizigo. Ikiwa uboreshaji utakuwa hautoshi, mashirika ya usafirishaji ya meli yataruhusiwa kutoza mpaka dola za Kimarekani 250 kwa faini ya chombo kilichochelewa kutolewa.

“Mdau yeyote ambaye atachelewa kuondosha mzigo atachukuliwa kuwa ndiye dhamana,” alisema Meneja wa Masuala ya Umma wa SUMATRA, David Mziray katika barua, akionya kuwa watakuwa dhamana kwa kulipa malipo ya ziada yatakayotozwa.

Unaonaje kuhusu makala hii? (Jumla ya Kura 1)

Dislike_icon(0)

(Sera za kutoa Maoni) *Inaonesha Maeneo yanayohitaji

Habari Mpya kabisa

Katika Mwangaza

Jisajili

Kura

Je, unadhania kupigwa marufuku kwa hotuba ya chuki na Tanzania kutakomesha mashambulizi dhidi ya makanisa na misikiti?

Angalia matokeo