Uturuki yatoa dola za Marekani milioni 365 kwa Somalia

Februari 23, 2012

  • + Toa maoni sasa
  • Chapisha
  • Panga upya Punguza Ongeza

Uturuki imechangia dola milioni 365 kama fedha taslimu na njia nyingine za msaada kwa Somalia kwa mwaka uliopita, alisema Waziri Mkuu wa Uturuki hapo Jumatano (tarehe 22 Februari).

Uturuki imekuwa ikiongoza jitihada za misaada kwa Somalia, ambapo ukame uliua watoto 29,000 mwaka jana, imesema katika taarifa yake Ofisi ya Mratibu wa Diplomasia ya Umma iliyo chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu. Nchi hiyo pia inashiriki katika mkutano wa London kuhusu Somalia ulianza hapo Alhamisi.

Katika habari nyingine, wafanyakazi wa huduma ya maji wa Uturuki wamefungua visima viwili ambavyo vitasambaza huduma hiyo kwa Wasomali 126,000 wanaoishi kwenye kambi za muda mjini Mogadishu, meneja wa mradi Ismail Sevim ameliambia shirika la habari la Uturuki, Anadolu, hapo Alhamisi.

“Watu wanaoishi kwenye kambi hii walilazimika kuchota maji kwenye kisima kilicho umbali wa kilomita mbili,” alisema Mehmet Citil, mratibu wa shirika la misaada la Uturuki nchini Somalia linaloitwa Helping Hand. “Sasa wamefurahi maana wana maji yao wenyewe.”

Unaonaje kuhusu makala hii? (Jumla ya Kura 2)

Dislike_icon(0)

(Sera za kutoa Maoni) *Inaonesha Maeneo yanayohitaji

Habari Mpya kabisa

Katika Mwangaza

Jisajili

Kura

Je, unadhania kupigwa marufuku kwa hotuba ya chuki na Tanzania kutakomesha mashambulizi dhidi ya makanisa na misikiti?

Angalia matokeo