Viongozi wa dunia katika Mkutano wa London watoa wito kuchuliwa kuhusu Somalia

Februari 23, 2012

  • 2 Maoni
  • Chapisha
  • Panga upya Punguza Ongeza

Maafisa kutoka nchi 50 na mashirika yalikusanyika London hapo Alhamisi (tarehe 23 Februari) ili kujadili mpango mkuu kwa serikali ya Somalia.

Waziri Mkuu wa Uingereza David Cameron, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani Hillary Clinton na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon walikuwa miongoni mwa maafisa waliotaka hatua zichukuliwe kuhusu Somalia, na kutahadharisha kuwa dunia “italipa gharama” kwa kukosa kushughulikia machafuko ya kisiasa, wanamgambo wa Kiislamu na maharamia, AFP liliripoti.

“Matatizo haya ya Somalia hayaiathiri Somalia pekee. Yanatuathiri sote. Ikiwa sote tunakaa pembeni na kuangalia tu, tutalipa gharama kubwa kwa kufanya hivyo," Cameron alisema wakati wa kufungua mkutano. “Ikiwa kila mmoja atashirikiana na wengine kufanya japo kitu kidogo, ninahakika kabisa kuwa Somalia inaweza kutatua matatizo yake na hatimaye kutimiza wajibu wake kama muhusika mkuu ndani ya Afrika na duniani.”

Clinton alisema Marekani itashinikiza juu ya vikwazo, ikiwa ni pamoja na marufuku ya kusafiri na kuzuia mali kwa wale ambao “wanaweka vikwazo” kwa ajili ya maendeleo ya serikali ya mpito, utawala ambao unamaliza muda wake mwezi wa Agosti.

“Kwa miongo mingi, dunia imekuwa ikishughulikia katika kile ambacho yungeweza kukizuia kisitokee Somalia – iwe ni mgogoro wake, njaa au majanga mengine. Sasa tunakabiliwa na kile ambacho tunaweza kukijenga. Fursa hii ni ya kweli,” Clinton alisema.

Vilevile aliomba ziada ya dola za Kimarekani milioni 64 kwa msaada wa kibinadamu katika eneo hilo ili kusaidia kuboresha maisha ya Wasomali wa kawaida, waliokumbwa na njaa na vita vya wenyewe kwa wenyewe kwa muda wa miaki 21 iliyopita.

Ban yeye aliutaka ulimwengu kujenga juu ya maendeleo ya hivi karibuni baada ya Umoja wa Mataifa kukubali kukiinua kikosi cha kulinda amani cha Umoja wa Afrika katika nchi kwa kupeleka zaidi ya wanajeshi 17,000, na baada ya wanamgambo wa al-Shabaab kutolewa kutoka mji muhimu hapo Jumatano.

“Tumefungua nafasi kwa ajili ya amani na utulivu Somalia. Ni nafasi ndogo, lakini inawakilisha fursa ambayo hatuwezi kuifanya tuipoteze,” Ban alisema.

Huko Mogadishu, wakazi walipeperusha bendera za Uingereza zilizotengenezwa kwa mkono ili kuonesha kuunga mkono kwa mkutano huo, kwa mujibu wa AFP, hata baada ya milipuko miwili kuripotiwa huko Baidoa, mji ambao ulitekwa upya kutoka kwa al-Shabaab hapo Jumatano.

Mkutano huo unawaleta pamoja maafisa kutoka nchi 40, ikiwa ni pamoja na viongozi wa Ethiopia, Uganda na Kenya, pamoja na Umoja wa Afrika na Umoja wa Kiarabu.

Cameron alisema kuwa dunia sasa ina kazi tatu kubwa: kuisaidia Somalia kuimarisha usalama, kufikisha misaada ya kibinadamu katika sehemu inayohitajika, na kuzisaidia juhudi za Somalia katika kujenga serikali wakilishi.

Waziri Mkuu wa Somalia Abdiweli Mohamed Ali alisema katika kipindi cha kuelekea mkutano, kuwa nchi yake ilikuwa “inaelekea katika kipindi enzi ya amani, cha amani, utulivu na hali ya kawaida”.

Raisi wa Somalia, maraisi wa majimbo yenye utawala wa ndani ya Puntland na Galmudug, kamanda wa wanamgambo dhidi ya al-Shabaab, Ahlu Sunna wal Jamaa walitia saini makubaliano yaliyoungwa mkono na Umoja wa Mataifa hapo Jumamosi, makubaliano yanayoelezea muundo wa serikali mpya itakauochukua nafasi ya serikali ya mpito hapo mwezi wa Agosti.

Unaonaje kuhusu makala hii? (Jumla ya Kura 8)

Dislike_icon(0)

(Sera za kutoa Maoni) *Inaonesha Maeneo yanayohitaji

Maoni ya msomaji

  • Jaamac
    March 19, 2012 @ 12:43:13AM

    Lengo lililotangazwa la mkutano wa London ni kukubali hatua za kutekeleza na kuunga mkono mchakato mpya wa kisiasa pamoja na kutoa msaada kwa maeneo mengi ya Somalia na kutoa fedha kwa misheni ya Umoja wa Afrika, pia kuchukua hatua za kufaa za kupambana na uharamia na ugaidi na kuongeza uratibu wa misaada ya kibinadamu. Lakini hii imeonekana wazi baada ya kuibuka kwa mgogoro juu ya utajiri wa mafuta na uranium vilivyogundulika Somalia hivi karibuni. Maneno haya yanaonesha kile kilicho nyuma ya ulazimishaji na upelekaji wa majeshi mengi zaidi ya kigeni nchini Somalia, uzuwiaji wa matumizi ya bahari ya Somalia na nyenzo za majini na kuendelea kwa operesheni ya uvuvi haramu na utupaji wa takataka zenye sumu. Somalia imesambaratika na kuangukia katika mzozo kutokana na ushindani juu ya malighafi na uongozi.

  • Salah Sayfudiin
    February 26, 2012 @ 01:52:03AM

    Hali katika Somalia ni mbaya sana. Kuna watu wapatao milioni 9 wenye njaa ambao hawamudu hata chakula chao. Watu wanaishi katika hali za kukatisha tamaa licha ya kuwepo malighafi tele zinazoweza kuwalisha. Wanamgambo wenye siasa kali waliwalazimisha watu kwenda vitani, vita ambavyo hakuna yoyote nchini anayejua vitakwisha lini. Upatikana kwa maji safi ya kunywa na dawa ni mchache. Iko haja ya kuja kuwaokoa watu wa Somalia kutokana na matatizo hayo. Hali sasa imedhibitika na kunahitajika vitu vichache kutoka kwa mashirika ya kibinadamu. Onyo langu ni kuwa iko haja ya kumaliza utapiamlo, ukame na vurugu.

Habari Mpya kabisa

Katika Mwangaza

Jisajili

Kura

Je, unadhania kupigwa marufuku kwa hotuba ya chuki na Tanzania kutakomesha mashambulizi dhidi ya makanisa na misikiti?

Angalia matokeo