Red_arrow

Ungependa kuifanya Kiswahili kuwa lugha ya chaguo lako, katika tovuti hii? |

Al-Shabaab waripotiwa kutwaa kituo cha redio cha Afgoye

Januari 20, 2012

  • + Toa maoni sasa
  • Chapisha
  • Panga upya Punguza Ongeza

Wapiganaji wa al-Shabaab wameripotiwa kutwaa redio inayoendeshwa binafsi ya Afgoye, wakimkamata na kumtorosha mtangazaji wa redio Ayub Yusuf Dalmar, mtandao wa habari wa IT News Africa iliripoti Alhamisi (tarehe 19 Januari).

Wakazi wa Afgoye wanaoishi karibu na kituo kinachomilikiwa binafsi walisema al-Shabaab wanaweza kuwa wamekilenga kituo kwa sababu ya mtazamo wake dhidi ya kikundi hicho, liliripoti gazeti.

Katika miezi ya hivi karibuni, al-Shabaab imeongeza kutoa amri za vikwazo kwa wakazi wa Afgoye, kilometa 30 kusini mwa Mogadishu. Mwezi uliopita, wapiganaji waliwaamuru walimu wa dini kusimamisha masomo shuleni ili kuhudhuria semina ya “maadili ya kiroho ya jihadi”, liliripoti gazeti.

Vilevile uongozi wa Redio Afgoye wala al-Shabaab hawakueleza kuhusu tukio hilo.

Unaonaje kuhusu makala hii? (Jumla ya Kura 0)

Dislike_icon(0)

(Sera za kutoa Maoni) *Inaonesha Maeneo yanayohitaji

Habari Mpya kabisa

Katika Mwangaza

Jisajili

Kura

Je, unadhania kupigwa marufuku kwa hotuba ya chuki na Tanzania kutakomesha mashambulizi dhidi ya makanisa na misikiti?

Angalia matokeo