Polisi wa Kenya wamepuuza tahadhari ya vitisho na kuona kama dhihaka

Januari 11, 2012

  • + Toa maoni sasa
  • Chapisha
  • Panga upya Punguza Ongeza

Ujumbe wa maandishi uliotahadharisha Wakenya kwa shambulio la ugaidi ambalo lingetokea karibuni limechukuliwa kuwa ni mzaha, polisi wa Kenya walisema Jumanne (tarehe 10 Januari).

Alisema ujumbe huo ulianza kutapakazwa kwa njia ya simu za mkononi jioni Jumatatu ukisema, “UN walitoa tahadhari muhimu ya tishio la bomu usiku jijini Nairobi. Tafadhali kuwa mwangalifu na wajulishe ndugu zako na marafiki zako.”

“Tahadhari hiyo yenye kujadiliwa haikutoka ofisi ya UN mjini Nairobi na kwa uelewa wetu hakuna upelelezi kama huo katoka katika vyanzo vya kuaminika,” alisema msemaji wa polisi Eric Kiraithe.

Kiraithe aliwasisitiza umma “kuendelea na shughuli zao na kuendelea kuchukua tahadhari za usalama wa kawaida kama walivyoshauriwa wakati wa maelekezo yetu ya kawaida au kama walivyoshauriwa na polisi wa maeneo ya wenyeji", kwa mujibu wa habari zilizotolewa na Redio Capital FM News ya Kenya.

Polisi walisema uchunguzi unaendelea wa kutafuta chanzo cha ujumbe huo wa maandishi.

Unaonaje kuhusu makala hii? (Jumla ya Kura 0)

Dislike_icon(0)

(Sera za kutoa Maoni) *Inaonesha Maeneo yanayohitaji

Habari Mpya kabisa

Katika Mwangaza

Jisajili

Kura

Je, unadhania kupigwa marufuku kwa hotuba ya chuki na Tanzania kutakomesha mashambulizi dhidi ya makanisa na misikiti?

Angalia matokeo