Julai 30, 2012
Uamuzi wa Al-Shabaab wa kuwaua wanachama wake watatu kwa tuhuma za kupeleleza kwa ajili ya serikali za kigeni kunaonyesha ukosefu wa imani ndani ya vyeo vya kikundi cha wapiganaji, wachambuzi wa kisiasa na waangalizi wanasema
Al-Shabaab ilisema watu watatu -- Ishaq Omar Hassan,miaka 22, Yasin Osman Ahmed,miaka 23, na Mukhtar Ibrahim Sheikh, miaka 33 -- walikuwa wanapeleleza kwa ajili ya Shirika la Upelelezi la Marekani na Shirika la Upelelezi la Uingereza MI6.
"Hassan na Ahmed wote wawili walihusika na vifo vya Bilal al-Berjawi na wengine watatu [wanachama wa al-Shabaab]," shirika hilo linalohusiana na al-Qaeda lilisema katika mtandao wake wa Twitter tarehe 22 Julai. "Wawili hao waliweka vifaa vya ufuatiliaji katika magari ya al-Berjawi & kaka zake ambayo waliyaongoza makombora yaliyoshambulia vitongoji vya Mogadishu."
Al-Berjawi, mwenye uraia wa nchi mbili za Lebanon na Uingereza ambaye alivuliwa uraia wa Uingereza, aliuawa katika shambulio la kombora mwezi Januari nje ya Mogadishu. Iliripotiwa kuwa alikuwa kamanda msaidizi wa al-Qaeda nchini Somalia.
Waliyoshuhudia huko Marka walisema watu hao watatu waliuawa na kikosi chenye silaha katikati ya mji.
"Wapiganaji wa al-Shabaab ilitumia vipaza sauti vilivyofungwa katika malori kuwaita watu kushuhudia mauaji na watu walipokusanyika uwanjani, dazani ya wapiganaji waliyofunika nyuso zao waliwafunga vitambaa machoni watu hao watatu na kisha kuwapiga risasi, wakiwaua hapo hapo," mkaazi wa Marka Mohamed Said, miaka 34, aliiambia Sabahi
Omar Dahir, mkurugenzi wa Kituo kilichopo Mogadishu cha Marekebisho na Mjadala, alisema matatizo ya al-Shabaab yanatokana na kuongezeka kwa mgawanyiko miongoni mwa wanachama na kunaweza kusababisha kusambaratika kwa haraka kwa kikundi katika siku karibu zijazo.
"Kuna kutojiamini ndani ya al-Shabaab, kwa kuwa kikundi hakiwaamini wanachama wake na sasa viongozi wake hawaaminiani," Dahir aliiambia Sabahi. "Uamuzi wa al-Shabaab kuwaua wanachama wake watatu huko Marka unaonyesha ukosefu wa imani ambao unakikabili kikundi."
"Hii inaweza kuwa mwanzo wa kuvunjika kwa mipango ya mapigano iliyoandaliwa ndani ya kundi hilo, ambalo tayari linasumbuliwa na mgawanyo mkubwa," Dahir alisema.
Alisema al-Shabaab inaweza kukimbilia kuwaua kwa siri wengi wa wanachama wake kwa kuogopa kuwa kufanya mauaji mara mingi mbele ya wananchi kunaweza kuyumbisha umoja wa kundi hilo.
"Kundi hili litamuua mwanachama yeyote anyeshukiwa kuwa na uhusiano na pande za nje kwa sababu wanaogopa kuwa mashirika ya upelelezi ya Ulaya yanaweza kupenyeza kwenye kundi hilo na kuwalenga viongozi wao wanaotakiwa," Dahir said.
Al-Shabaab ilisema katika mtandao wa Twitter kuwa imezindua kampeni kubwa ya kukabili upelelezi ili kusafisha nchi kutokanana na majasusi hao .
Mwaka uliopita , kiongozi wa al-Shabaab Mualim Hashi Mohamed Farah alisema Kitengo cha upelelezi cha Ulaya kimepenyeza kwenye safu ya maaskari wa al-Shabaab, na mawakala wa pande mbili wanaojifanya kuwa wapigananaji wa vita vitakatifu.
Huu sio muda pekee kwa al-Shabaab kuwaua washirika wake waliotuhumiwa kwa kupeleleza kwa niaba ya mawakala wa upelelezi wa Kimagharibi. Al-Shabaab ilimuua makamu wa kiongozi wao mkuu wa upelelezi, Ahmed Ali Hussein, pia anajulikana kama Ahmed Keyse,mwaka 2010 kwa "upelelezi " wa serikali za kigeni.
Tarehe 27 Julai, al-Shabaab ilisema iliwakamata "wapelelezi watatu wa TFG" ambao kwa sasa wanahojiwa. "Kama watatiwa hatiani watu hao watatu watauawa hadharani," al-Shabaab ilisema katika Twitter.
"Vurugu za kujiamini zimetawala katika sura ya nchi ndani ya kundi la al-Shabaab,ambazo zimesababisha mauaji ya washirika wake," alisema Abdirahman Mohamud, mwangalizi wa makundi yenye msimamo mkali.
Tangu Marekeni ilipotangaza tarehe 7 Juni kwamba itatoa zawadi ya hadi Dola za Marekeni milioni 33 kwa taarifa zinazowahusu wapi walipo viongozi saba wa ngazi ya juu wa al-Shabaab, viongozi wanaotafutwa wamejificha dhidi ya sio tu kikosi cha upelelezi lakini pia dhidi ya macho ya jamii na washirika wao.
"Viongozi wa al-Shabaab sasa wana wasiwasi kwamba Marekeni kutoa tuzo ya fedha kutasababisha kutoa msukumo kwa baadhi ya washirika wa kundi, ambao watahamasishwa na uroho waa pesa, kuwasaliti viongozi wao na kutoa taarifa kuhusu walipo ili wajipatie zawadi za fedha," Mohamud aliiambia Sabahi.
"Kwa maoni yangu huo ni motisha kwa uamuzi wa al-Shabaab hivi karibuni kuwaua washirika wake watatu kwa tuhuma za kufanya upelelezi kwa niaba ya mawakala wa kipelelezi wa Marekani na Uingereza," alisema.
Mohamud alisema al-Shabaab imegawanyika katika kambi mbili, na kila moja "itafanya ukatili" dhidi ya nyingine.
Mwezi Machi, kiongozi wa al-Shabaab Hasan Dahir Aweys alilaumu kikundi cha wanamgambo kwa kuwaua wananchi bila ya malengo kwa jina la kiislamu na kwa kushirikishwa kwake na al-Qaeda. "
Kundi lenye msimamo mkali la al-Shabaab lilifanya mauaji mengi katika miaka michache iliyopita, yakilenga sio tu washirika wake lakini pia na wananchi wengi wa Somalia waliotuhumiwa wakifanya kazi na upelelezi kwa ajili ya mawakala wa upelelezi wa Kimagharibi au wakishirikiana na majeshi ya serikali ya Somalia au Umoja wa Afrika," alisema Abdullahi Osman, mchambuzi wa masuala ya kisiasa na mtaalamu katika masuala ya vikundi vya waislamu wenye msimamo mkali nchini Somalia.
Osman aliiambia Sabahi kwamba al-Shabaab wanawafanyia ugaidi wananchi wa Somalia na wanatishia kuwaua wale ambao wanashirikiana na serikali au Umoja wa Afrika waliopo nchini Somalia.
Alitoa wito kwa serikali ya Somalia kuimarisha jitihada zao ili kuyakomboa maeneo yaliyobakia chini ya udhibiti wa al-Shabaab kumaliza uhalifu wa kuchukiza unaofanywa na kikundi hicho.
"Al-Shabaab itaendelea kufanya vurugu za kutokuwa na hadhari na kutochagua kwa uangalifu dhidi ya wananchi wa Somalia hadi kundi hilo litakapotolewa nchini," alisema.
Wabunge wameondoa hoja yao inayomtaka Waziri Mkuu Abdi Farah Shirdon na baraza lake la mawaziri k...
Rais Ahmed Silanyo wa mkoa wa Somaliland alikutana na Mwakilishi Maalum wa Umoja wa Ulaya kwa Som...
Ukiritimba na ukosefu wa ufanisi katika bandari ya Dar es Salaam unaigharimu Tanzania na nchi jir...
Viongozi wa mkoa wa Puntland walikutana siku ya Jumanne (tarehe 21 Mei) kuwashajiisha wanawake ku...
Wanajeshi wa Somalia na wa Misheni ya Umoja wa Afrika nchini Somalia (AMISOM) waliwakamata zaidi ...
Rais Ismail Omar Guelleh wa Djibouti alijadiliana ushirikiano wa kimkakati na Kanali Saleh Ben Na...
Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta, vikosi vya usalama na mahakama vinapaswa kuomba radhi hadharani kut...
Waziri Mkuu wa Djibouti Abdoulkader Kamil Mohamed alitoa wito wa kuongezwa kwa ushirikiano katika...
Baadhi ya wabunge wa Somalia wameitupilia mbali hoja ya kumtaka waziri mkuu na baraza lake la maw...
Wabunge wa upinzani walidai kwamba serikali ya Tanzania imekuwa ikibana uhuru wa kujieleza na kud...
(Sera za kutoa Maoni) *Inaonesha Maeneo yanayohitaji
Maoni ya msomaji
Wacha niseme - kutafuta msaada wa Mungu - kwamba taifa la Kiislamu la Somalia limeathiriwa na gengi hili la wahalifu ambalo linajificha chini ya mwavuli wa Uislamu na kurejesha nyuma misingi mikuu ya dini zote zinazoamini Mungu mmoja ambayo wamekubaliana. Kikundi hiki kinafuata mkabala ule ule ambao umekuwa ukifuatwa na Kharijit, ambao wanathubutu kutoa maisha ya watu wasio na hatia kutokana na shutuma zisizo sahihi tu. Ina maana gani kudai kwamba Uislamu umeasisiswa kwa kuwakata vichwa watu wasio na hatia? Kwa ajili ya Mungu, mnapaswa kujifunza historia ya Umma huu mtukufu (taifa la Waislamu) ili kujihakikishia wenyewe juu ya uhalifu wa al-Shabaab na jinsi unavyoupaka matope Uislamu kwa njia ambayo ni tafauti na sura yake ya kweli. Wacha nimalizie kwa kusema hili: kile kinachotokea miongoni mwa al-Shabaab sasa ni mwanzo wa kisasi cha Mungu kwa taifa la Kiislamu. Utokomeaji wa al-Shabaab uko karibu, na waumini watafurahia siku hiyo na kuwa na furaha juu ya uokozi wa Mungu.
Hivi uislamu ni kumsaidia Mungu kuwaua watu wenye dhambi kama wao Al Shabaab wanavyowaita mkafiri, Hivi huyo ni mungu wa namna gani anayehitaji msaada wa binadamu aliye muumba ili amfanyie kazi ya mauaji, basi Mungu huyo wa waislamu hana uwezo na kama ni hivyo kuna sababu gani ya kufuata kitu kisicho na uwezo.hivi ndivyo Quran ifundishavyo ni aya zipi hizo ambazo Mtume Mohammed na Mola wameziteua zifundishwe kwa watu kuwa makatili. Hivi kweli hata kwa akili ya kibinadamu mtu mwenye utashi anaweza kufanya mambo ya kijinga kama hayo, halafu eti Mwenyezi Mungu anafurahia huko ahera? Dini hii ni dini yenye tatizo la kisaikolojia kama sio dini yenye muongozo washetwani .Angalieni sana enye waja wa mwenyezi Mungu mnaotaka ahera na huko mnau a ndugu zenu kwa faida zenu binafsi upo wakati Mwenyezi Mungu atasema na ninyi
kumbuka kuuwa ni dhambi ngugu zetu waislamu mzoea kuuwa kwa kisingzio kuwa mnatetea imani yenu. naamini kuwa mungu ni mwema kwa wote pia ni wa amani. imani ya shetani ndio ya kuuwa sio mungu.kuuwa watu wasio na hatia haipendezi machoni pa mungu na watu. sasa hivi alipo mwislam anadhaniwa kuwa ni gaidi au jambazi au mwizi,ona wanavyochoma makanisa kule tanzania
Ninamuomba Mungu awaongoze katika njia iliyonyooka kwa vile wamepotea.
Niliangalia filamu iliyochezwa na watu watatu. Kwa kweli ni wanaume, nashangaa na vipi waliicheza. Wote watatu walihojiwa na walisema ukweli. Nimeogopeshwa na jinsi gani wamefanya vitu hadi sasa. Hata hivyo hadithi yao ilitoka baada ya kumaliza mtu wa tatu, Mukhtar. Walilipwa dola 7000 tu kwa masuala yote mawili lakini sasa wameshafariki. Naomba Mungu atulinde. Kwa kweli watu hawa wanafuatwa fuatwa.
Al-Shabaab watashinda na hivyo hawafai kuwa na pupa. Utawala huu mpya ni tawi la kisiasa tu la Al-Shabaab na hamfai kudanganyika kwa kuwajua.
Mungu ailinde jamii ya Wasomali kutoka kwa kundi hili potofu. Amin!
Al-Shabaab ndio tatizo pekee linalojaribu njia mbaya kwa maisha ya Wasomali. Wasomali wanapaswa kufikiri kama watu waliostaraabika na hawapaswi kujali juu ya Msomali yeyote anayeabudu dini nyengine kama vile Ukristo. Kila mtu anapaswa kupewa uhuru wa dini na uhuru wa kuabudu. Ikiwa unahisi wazo hili ni baya kwa hivyo wewe utakuwa mwanachama wa al-Shabaab na huwezi kujificha.
SABAHI NI YA KENYA NA HILO LINAJULIKANA. NYINYI NI MAKAFIRI NA WAUNGAJI MKONO WA MAKAFIRI. TOKENI, NYINYI WEZI MNAOFANYAKAZI KWA AJILI YA MAKAFIRI.
Mungu atuongoze katika njia iliyonyooka, Mungu akipenda. Hali ya sasa inahitaji maombi yetu kwa Mungu ili atuokoe. Tujiepushe na kile ambacho Mungu amekataza tusikifanye. Mungu anawajua maadui wa dini na waumini pia wanawajua maadui. Ukweli utakuwa wazi kwa sababu Mungu amewaumba watu na Yeye atawatenganisha. Mungu tayari alisema mahali ambapo atawatenganisha watu wake. Jaribu kwa bidii na kuweka imani yako kwa Mungu na kuwa na imani kwake Yeye, Mungu akipenda. Maadui wa Mungu hawatakuambia chochote.
Wakati wa al-Shabaab umemalizika, serikali mpya imezaliwa usiku huu na tumshukuru Mwenyezi Mungu.
Binafsi nadhani ikiwa suala la al-Shabaab lingekabiliwa kwa makini, watu waliotafrika ambao walidharauliwa wangekuwa wameshakombolewa muda mrefu na mtu huhisi kuwa suala hili ni mchezo tu kwa sababu kwa karibu ya mwaka majeshi ya serikali yameshindwa kuigusa Kismayu. Kwa hivyo, ikiwa suala hili ni sahihi, kitu gani kinazuwia? Binafsi sina jawabu kwa swali hili.
KAMA WAPO WAISLAMU WA KWELI WANAOELEWA VYEMA DINI YAO, KWA NINI HAWAJI JUU KUPINGA VITENDO HIVI VYA KISHENZI VYA AL-SHABAAB? BADO SIJAONA JINSI UISLAMU UNAVYOFAHAMIKA KUWA WA AMANI. WALA MTUME WAO AU KORAN HAILAANI VURUGU. TENA, NI WAOGA WANAJIHUSISHA NA VURUGU KWA NJIA AMBAYO MTU SHUJAA HAFANYI. NINAUDHARAU UISLAMU NA KILA KITU KINACHOKISIMAMIA.
Kinachowafanya watu watofautiane na wanyama ni kitu kimoja, “Binadamu anaweza kufikiri” kwa hivyo ni kufikiri kumruhusu kaka/dada/mama/baba…n.k. kuteseka wakati wewe ndio sababu ya tendo hilo? Wanaume na wanawake, tudumishe amani na upendo.
Asante Sabahionline kwa kuripoti kuzuri. Al-Shabaab wanatokana na mfalme wa ukatili; Shetani. Lao ni wizi, mauaji na uharibifu. Yesu alikuja kupeana maisha na maisha kwa wingi. Wasomali tafadhalini, mwelekeeni Yesu kwa kutibiwa ardhi yenu na maisha kwa wingi. Mtawazeni kuwa mfalme wa nchini yenu, Amin.
Maombi ya amani kwa watu wote. Kwa muda mrefu nilikuwa ninadhani kuwa neno UIslamu linamaanisha amani ... sasa linaonekana kama vitisho. Watu wangapi wanahisi hivyo hivyo wanapoona mwanamke aliyevaa buibui anaingia dukani? Kinachotokea ni watu kununua kwa haraka haraka na kuondoka kabla ya kushuhudia umwagaji wa damu, hiyo ni kama utakuwa na bahati ya kutosha.
Naamini kuwa sote kwa umoja wetu tutawashinda maadui. Kila kitu kinawezekana kwa Mungu.
Kuna tatizo gani katika ulimwengu wa Kiislamu? Kutokuwepo na utulivu duniani kote siku zote kunasababishwa majamaa hawa Waislamu kuanzia nyakati za Goliath wa Palestina hadi leo. Nyinyi watu mnataka nini? Mmeifanyia ugaidi dunia nzima kwa kisingizio cha kupambana na Marekani na washirika wake kwa sababu ya kiburi, kwa hivyo? Samahani, mnatumiza baadhi ya tabiri katika Biblia licha ya ukweli kwamba mmepiga hatua ya propaganda. Ni za asili lakini subiri kwa kupepesa jicho, nyinyi ulimwengu wa Kiislamu na wengine kama binadamu mtateketea daima kwa sababu kwa kuifanya dunia ambayo Mungu aliimba kuwa ikalike kwa amani lakini mmeifanya kuwa motoni kabla ya wakati ulioteuliwa. Angalieni kile mnachofanya kwa jina la Jihadi, mauaji ya watu wasio na hatia kupitia kujitoa muhanga kwa sababu ya itikadi za kishenzi za kuingia peponi. Nani aliwaambia kuwa kuwaua watu wasiokuwa Waislamu kama mnavyouita ulimwengu wa wasiokuwa Waislamu ni makafiri (neno lisilo na maana) kwamba mtazawadiwa pepo ya maisha?. Waungwana, Mungu ni mmoja ambaye aliumba dunia hii nzuri na kwa hivyo hamna haki ya kuwahukumu watu wengine kwamba vita vyenu ni kuwaona wakazi wa dunia yote wanasilimishwa. Kitu mnachokosea sana, mtajuaje kama nyinyi ndio mnaofanya mema mbele ya Mungu, kwa vile ni yeye tu. Acheni kuwahukumu watu wengine kwa kuwaua wakati nyinyi hamjui mustakbali wenu. Angalieni wale kwa jina la Uislamu, vijana na elimu yao yote, walifanya tarehe 9/11. Ni aibu, waliangamia na pia waliangamia watu wengine wengi wasio na hatia na ajali nyingi. Asanteni.
Mungu isaidie Somalia ili kushinda mateso.
Sasa niwazi kuwa al-Shabaab wameshindwa na hii ni kutokana na juhudi za watu wa Somalia pamoja na majeshi. Tangu kushindwa, maisha yanarejea kuwa ya kawaida na sasa watu sasa wanashughulikia kuijenga upya nchi yao. Serikali pia imeimarika kwa usalama.
Mungu rejesha amani SOMALILAND.
Mungu Mwenyezi umewaumba binadamu wote katika sura yako mwenyewe. Jaalia busara zako katika nyoyo zetu na tusaidie kukumbuka kuwa sisi ni kaka na dada bila ya kujali tofauti zetu za imani.
Ugaidi wa Somalia unaendeshwa na al-Shabaab ambao wamekuwa wakitenda baadhi ya matendo ya uangamizaji na yasiyo ya kimaadili kwa watu wa Somalia na majirani zao. Walikuwa wanakata viganja vya yeyote aliyejaribu kutokukubaliana nao na pia kama njia ya kuwadhibiti na kuwatawala. Lengo lao kuu lilikuwa maeneo ya umma na mikusanyiko ya kijamii ambapo walifanya mauaji ya mabomu ya kujitoa muhanga na kuua mamia ya watu wakiwemo watoto wadogo. Kikundi hiki cha kigaidi kiliendelea kuteka nyara meli bahari kuu na wakati wa utekaji baadhi ya mabaharia waliweza kuuliwa, na baadaye kuomba kikomboleo. Al-Shabaab ilikuwa inazuwia kwenye miji iliyokuwa inayadhibiti isifikiwe na msaada wa chakula na madawa, kulikopelekea mateso yasiyosemeka na vifo vya maelfu ya watu nchini Somalia. Utekaji nyara wa watoto na kuwafanya askari kulikuwa ni ukiukwaji mkubwa wa haki za binadamu. Magaidi waliwageuza Wasomali kuwa wakimbizi na watu wa ndani waliokimbia makazi yao na kuwasababishia mateso na machungu. Walivunja viungo vingi vya familia kutokana na kuhamahama na mauaji, na watoto wengi kubaki mayatima na wanawake kubaki wajane. Kulikuwa na umwagaji damu mkubwa katika nchi ya wasio na hatia wakati kikundi wakiteketeza na kuua kila kitu njiani kwao.
NAAM! MAISHA NDIO KWANZA YAMEANZA. KARIBUNI VITA VITAMALIZIKA NA VYENGINE VITAANZA. SISI NI BINADAMU AMBAO KIMAUMBILE TUNAANDAMWA NA MIZOZO. UTAWALA MBOVU WA SOMALIA NDIO SABABU YA VITA. SOMALIA INAHITAJI KUTAWALIWA KWA WAKATI FULANI, KABLA YA KUPEWA UHURU.
al-shaababu kama mungu anatenda miujiza sasa miujiza inatendeka kwenu hakuna damu inamwajika isiyokuwa na hatia isiume sasa niwakati wa kulipa kila baya na jema mlilolifanya enyi wANA WA MUNGU OGOPENI ZAMBI ZA MAUAJI ZISIZO NA HATIA
Kila chenye mwanzo kinamwisho,enyi wasomali mkiona mateso yanazidi,jueni hakika kuwa ukombozi un akaribia. sasa hapo fale inafitinika. alshababu wekeni silaha chini,muogopeni Mwenyezi Mungu!
ABADANI ASILANI USIUWE KWA JINA LA DINI ... MTAANGAMIZWA NA KUWA HAMNA MAANA!!!!
Sabahionline ni CHOMBO CHA HABARI CHA MAREKANI na kinadhibitiwa na AFRICOM huko Djibouti. Kwa hivyo, makala zake hazina msingi wowote na ni za uongo. Wantumia madondoo yasiyo ya ukweli kutoka watu wasiokuwepo. Makala zake hazitayarishwi kwa maadili na kanuni za vyombo vya habari juu ya kutopendelea upande wowote.
Endeleeni, AL-SHABAAB
Baba yetu uliye Mbinguni jina lako lisifiwe. Somalia ni nchi yetu, ewe Mungu iokoe dhidi ya hatari hii. Nguvu na Uwezo wako utawale. Viharibu na vifadhaishe vikosi vya waovu na watu wabaya na imarisha nguvu zote za wenye haki na sheria na katika ardhi ya Somalia. Hii ni dua yangu pamoja na Wasomali wazalendo kwa jina lililo juu ya majina yote mengine, jina la YESU KRISTO, Amen!
Al shabaab ni adui mwoga ambaye katu hatatokeza hadharani ana kwa ana na kulala hadi kila kitu kimetulia ndio wanashambulia tena. Kushindwa sio chaguo na hakuna njia, wakubali tu kuwa wameshindwa. Napenda kuwashauri wote wawe na tahadhari wakielewa kuwa shujaa daima hafi pekee yake. Hata kama kikundi kinaonesha kushindwa kidogo wanaweza kufanya kitu kikubwa wakati hatimaye watasalimu amri. Al-Shabaab hawatashindwa, bado hadi kila kitu kimalizike. Tunaweza kuyaamini maneno hayo ikiwa yatatoka kwa jeshi linalowapiga al-Shabaab na sio kutoka kwa al-Shabaab wenyewe. MWISHO. "TUTARAJIE MEMA ZAIDI LAKINI TUJITAYARISHE KWA BAYA ZAIDI".
Je kuna mtu anaweza kutuambia historia ya "al-Shabaab"? Kwa nini wanapigana, na nani hasi?
Wale walio katika upande wa haki watashinda. Mungu analinda na kuonesha huruma kwa waja wake kwa uwezo wote na hakutakuwa na nguvu za kutosha kulizuia hilo.
Ni jambo la kuhuzunisha wakati wale mabwana wa vita wakitaja sisi ni vikundi vya Kiislamu.
Hongera al-Shaabab, hivi karibuni tutaungana nanyi na tutashinda vita Mungu akipenda, sio tu katika Somalia bali Afrika ya Mashariki yote. Hamna chochote cha kupoteza. Mwenyezi Mungu (SW) awalinde na kuwaongoza kuelekea ushindi.
WAJINGA WA KUTUPWA, AL-SHABAAB, MWAKANI MTASHINDWA
Al shaabab ni hatari, wanafahamu ufumbuzi wa tatizo ni kuua, mafundisho mengine yana madhara na haya ni baadhi ya madhara hayo . Ni vyema dunia ikaungana kumaliza kundi hili pamoja na mshirika wake al qaida
Yesu tu ndiye anayeweza kuleta utulivu katika nchi ya Somalia. Amri inasema: USIUE, kwa hivyo kwa nini basi kuua. Hii ni moja ya sababu zilinifanya kutoka katika Uislamu na kujiunga na Ukristo.
Mungu ni Mkubwa, mwisho unakaribia, kwa hivyo Mungu tusaidie
Sisi watu walio karibu na Somalia na wananchi wa Somalia tunahitaji kuungana mkono kwa sababu kikundi hiki kilikuwa tishio kwa kanda hii. Hongera TFG
Ingekuwa bora kuacha vurugu kwa sababu hata Mungu wetu haipendi hali kama hiyo kwa watu wake.
Ingekuwa bora kuacha vurugu kwa sababu hata Mungu wetu haipendi hali kama hiyo kwa watu wake.
Jah Mwenye Uwezo awazawadieni kwa kazi nzuri mnayofanya.
AL-SHABAAB, SIKU ZENU ZA DAMU ZINAHESABIKA. MNAUA WAISLAMU NA MNAJIITA WENYEWE WAISLAMU. MTAKWENDA JEHANAMU MOJA KWA MOJA ...... HAKI ITATAWALA.
Natamani kuwa ndugu zetu wa Somalia watawafuata wale wanaotetea siasa za wastani, ambao wanauelewa kwa upana juu ya Uislamu. Wanazuoni lazima pia watoe hotuba misikitini ili kueneza Sharia halisi ya Kiislamu na kukabiliana na kuibuka kwa wahubiri wa itikadi kali ambao wanahimiza ghasia katika hotuba zao. Hata hivyo, hatua hii haitafanyika kama serikali na hasa vikosi vya usalama havitaamini kwamba kuna tofauti kubwa kati ya Uislamu na huruma zake na kuvumiliana kwa upande mmoja na mawazo ya msimamo mkali kwa upande wa pili. Napendekeza kuanzishwa kwa kozi za kuwaelezea watu wa vikosi vya usalama mtazamo sahihi kuhusu msimamo mkali na kuwafundisha kwamba wao ni kama wagonjwa ambao wanahitaji matibabu badala ya kuwashughulika kama wahalifu. Mitazamo tofauti itakuwa msingi wa matibabu tofauti. Kama tutawaona wao kama wahalifu, basi tutakuwa tunataka kuwatendea ukatili na unyanyasaji na tunapaswa kuwaadhibu. Hata hivyo, kama tunaona wanahitaji mazungumzo na kutibiwa, matibabu yatakuwa tofauti kwa sababu tabia zote za mtu ni msingi juu ya imani yake. Tabia mbaya hutokana na imani potofu na hawatabadilika bila kujali ni kiasi gani wanakabiliwa na shinikizo la kimwili au kisaikolojia. Kufungua mlango kwa wanaotubu na huruma na kuwapa hisia kwamba yeyote anayetaka kutubu atasamahewa bila kushinikiza wengi wa watu hao watarudi katika njia iliyonyooka. Mwenyezi Mungu Mtukufu anasema (maana yake): {Sema: Enyi waja wangu walio jidhulumu nafsi zao! Msikate tamaa na Rehema ya Mwenyezi Mungu, Ambaye husamehe dhambi zote. Kwa hakika! Yeye ni Mwenye kusamehe, Mwenye kurehemu}. Kwa hivyo, waja wa Mungu wanapaswa kutenda katika njia hii kwa sababu kubwa zaidi. Hii pia inawahusu wasamehevu na watenda maovu na hii lazima iwafanye kuacha kurudia makosa hayo hayo.
Nitakwenda kupambana nao!
Allah awafanyie wepesi wasomali amani ya kweli ipatikane na madhalimu wote washindwe.
Sisi ni dunia ya wazima moto. Tunashughulikia matatizo tuliyoyasababisha wenyewe. Kwa vyovyote vile, hata hivyo, uhalali wa KDF nchini Somalia una sababu lakini ukweli ni kuwa Somalia itakuwa huru kutokana na vitisho vya al-Shabaab iwapo Taifa lote litaelekeza juhudi zake katika kuelimisha na sio katika silaha kwa halaiki. Tumai kuwa kila kitu kitakwenda vyema karibuni sana kwa ajili ya maisha ya binadamu. Dini ni kisingizio, kwa kweli daima haikuwahi kuzaa ugomvi hapa lakini...
Mungu anataka kuwa nusuru na maafa makubwa acheni hizo
Siamini kama watu hawa ni Wasomali kwa sababu hawajali hatima ya Somalia. Watu hawa ni wauaji. Baadhi ya Watanzania wanaamini katika itikadi za al-Shabaab, hii ni hatari, hawako tayari kujifunza kutoka Somalia. Sisi huku Tanzania mara nyingi tunapokea Wasomali waliokimbia nchi yao, lakini siwafahamu baadhi ya Waislamu wa Tanzania, kwa nini hawajifunzi kutoka kwa wa Somali?
kumbuka enyi waislamu acha kuuwa watu ovyo. mungu ni mwema na mungu ni wa wote lakini ninyi mnauwa watu eti ndipo mtafika mbinguni.kama ni hivyo basi mungu angeumba wailamu peke yao.lakini hakufanya hinyo.anajilipua au kulipua wengine atambue mungu ndiye wa kutoa uhai si bndamu.tumechoka kuuwa watu ovyo
SIKUBALIANI KABISA NA WALE WANAOSEMA KUWA AL-SHABAAB WANA HAKI YA KUUWA YEYOTE AMBAYE HAKUBALIANI NAO....
Sio watu wa Somalia tu wanaoteseka bali hata fisi pia ambapo al-Shabaab imefanya ulaji wa fisi ni halali hadharani.
Kikundi hiki lazima kisafishwe kutoka uso wa dunia.
HONGERA KDF, sasa tunahisi tunalindwa. Maisha yetu kama Wakenya yamo mikononi mwenu. Tunawaamini. Tafadhalini endeleeni.
there is and wahat you fori of mimi wewe by weot na makumbati nyangi mara
Katu al-Shabaab hawatashinda.
Siku zao zinahesabika.
Wanafiki hawana nafasi katika Jihadi au katika Uislamu. Wakithibitika kuwa ni watu wabaya, waacheni wachinjwe. Wale walio imara tu lazima wabakie katika vita.
Hii inaashiria mwisho wa kila kitu. Al-Shabaab, siku zenu zimekwisha. Nyinyi msalimu amri TU kwa ajili ya maisha yenu na maisha ya kaka na dada zenu kwa sababu wakati umefika na ni WENYE KUMCHA MUNGU tu watakaosimama.
Serikali lazima ilisimamie suala hili na kuingilia kati wakati hali itakapokuwa mbaya zaidi ili kulinda maisha ya watu, mali na maendeleo yaliyokwishafikiwa na jamii. Kwa kuhitimisha, tunahitaji kuunganisha juhudi zetu katika kuzileta familia pamoja.
Majambazi hawa wamechanganyikiwa kwa sababu majeshi yetu yanawakaribia, sasa badala ya kupigana kama walivyoanza kuichokza Kenya kwa kufikiria kuwa askari wetu hawawezi kupigana, sasa wameshughulika kuuana wao kwa wao na kuiweka mikakati yao kuwa mchafukoge kabisa! Kwa kweli Mungu anawahukumu. Kikundi hiki cha majambazi kitamalizwa, ni suala la wiki chache tu kwa ndugu zetu wa Somalia kupata uhuru wao.
Kwa kweli kitendo cha Hao jamaa kuuana nfikiri ni neema kwa Wasomali maana kila kukicha Wasomali wanakimbia mapigano na kuingia Nchi za jirani kama wahamiaji haramu, hivyo basi ni bora hao elshabaab wauane ili iwe rahisi kuwakamata wakishapunguzana ili sheria ifuate mkondo wake
Kwakweli hakuna ambae haoni wala hasikii jinsi ndugu zetu somalia wanavyoteseka na ugaidi na mauajia ya raia wa somalia -ombi langu tumeona Tanzania umekomboa nchi nyingi sana ningeomba Tanzania ijaribu kuikomboa somalia kwa hawa jamaa al-shabaab najua Tanzania inaweza.
Mi nadhani wa kulaumiwa si alshabab wa kulaumiwa ni mataifa ya kimagharibi,ambayo yamepandikiza chuki dhidi ya uislamu na waislamu,waislamu na wakristo wameishi kwa karne nyingi wakitofautiana imani,nakushirikana katika mambo mengi na si VITA vita ya somalia imekuja pale mataifa ya kimagharibi yakiongozwa na marekani kusaidia waasi kuidondosha Serikali Halali ya kiislamu.Sasa mdadhara yake ndo haya wanakufa watu wasio na hatia mataifa haya yamekaa kando na kuzidi kufanya biashara za silaha,na majaribio ya silaha zao mpya walaumiwe WAMAREKANI NA WASHIRIKA WAKE HII NI JIHAD WALA HAINA SHAKA, MUNGU ATASAIDIA AMANI ITAPATIKANA NA HESHMA ITAKUWEPO TU.
Dada na kaka zetu katika jeshi watuondolee majangili hawa mara moja. Waendelee na kazi nzuri kwani inayoonesha mafanikio mazuri. Tuko nyuma yenu kwa asilimia 100. Shukurani zetu za dhati na dua zetu kwenu. Tuwasafishe kabisa duniani.
MUNGU, ubarikiwe.
Tutashinda vita hivi, Mungu akipenda. Mungu yuko upande wetu.
Search Al-Shabaab kuwaua wanachama wake kunaashiria matatizo makubwa - Sabahionline.com
Ninaamini sana kuwa Serikali ya Mpito ya Shirikisho itashinda mapigano kwa vile Mungu daima yuko pamoja nayo. Wanachama mashetani wa al-Shabaab wataangamizwa motoni.
kama kuna dini inayoruhusu kuuwa hiyo ni dini ya shetani. mara nyingi watu wajiita waislamu na wanauwa watu bila huruma, kwa kujilpua kwa kuwachinja, kuwatwanga mawe hadhrani.mtu anapojilipua huuwa hat wasio na hatia tumeshuhudia kenya, nigeria, uganda n,k.naomba nifahamshe mtume mhamadi alihubri kuuwa watu ovyo na je kuna tofauti gani kati ya ugaidi na uislam?je mungu wetu ni wa kuuwa au wa kuponyesha
Asanteni vikosi vyetu vya Kenya kwa kazi nzuri mnayofanya.
Kamwe al-Shabaab hawatashinda. Naipongeza serikali ya kenya kwa maamuzi yao kuisaidia somalia katika vita ili kuing’oa al-Shabaab na kuokoa maisha ya watu wa Somalia. Nadhani hii ni changamoto kwa nchi zingine za Afrika kuwa na mwamko kama huo kuungana na kuzima mapigano hayo kwa hali na mali. Poleni wasomali kupoteza ndugu zenu.
Lini mtaacha tabia ya kuuana wenyewe kwa wenyewe? Angalieni mnatoka wapi na mnakwenda wapi...sitisheni mapigano!!!!!!!!!!!!!!!!
Shukurani kwa Mungu kuwa mara hii sio Muhamed, Muhamed Kamau, Muhamed Njoroge, Muhamed Mutizo au Muhamed Otieno. Tafadhalini vijana wetu rejeeni nyumbani katika vijiji vya Kangema, Masako na Siaya na mtubu tu vyenginevyo vijana hawa wendawazimu wanaoitwa al-Shabaab wataendelea na kukata tamaa kwao na watawauweni nyote wanaowaiteni majasusi. Tumeshawasameheni licha ya kuwa mliwapiga mabomu mama, dada zenu, n.k.
Hawa maalshabbab bana si wajikate tu ama wajitie kitanzi coz wanalose n its my hope they lose.
Al-Shabaab huwa wanapata silaha kutoka wapi? Naamini kuwa wanapata msaada kutoka mataifa yenye nguvu ambayo hayana haja ya amani nchini Somalia. Mataifa haya yanafaidika katika uuzaji wa silaha. Uislamu unafundisha wazi kuwa yeyote anayeua mtu lazima na yeye auliwe. Sifahamu Al-Shabaab wanayatafsiri vipi mafundisho haya.
Alshabab wanatoa wapi silaha? Mimi naamini kuna mataifa makubwa yapo nyuma ya Alshabab na Koo za kisomali.Mataifa haya yanafaidika kwa kuuza silaha.Islamic teachings inaeleza bayana kuwa,Atakayeua mtu basi naye auawe.Sijui Alshabab wanatafsiri vipi mafundisho haya.
Kwa mimi sio wazuri kwa sababu wanawaua watu wasio hatia kila mara.
Dini na imani za kidini, na utekelezaji wake ni mambo ngumu, wote na baadhi wanahitaji kutambua na kufahamu kuwa dini ni suala binafsi na la ushirikiano na kwamba kila mmoja wetu anahitaji kuelewa la sivyo tutaangukia katika uchoyo na mafundisho hatari na yanayopotosha, fikra potofu ambayo itamchukua mtu milele. Binadamu wazingatie upana huu wa dini hata kama tunaachagua kuabudu muumba wa kweli wa pepo, ardhi na vyote vinavyoishi na visivyoishi. Binadamu wote pia wakubali ukweli kwamba mwisho wa maisha yetu hapa duniani utakuwa mmoja juu ya Mungu mmoja na kwamba binadamu wote kwa jumla mafundisho yanayokubalika kwa jumla katika dini zote za ulimwengu. Kwa hivyo, sote tuna jukumu la kuhakikisha kuwa sisi ni watu wa dini ya kweli iliyojikita katika imani binafsi na sio katika mafundisho ya watu wengine na kufahamu dini na udini unahusu nini.
Nashindwa kujua hasa kinachopiganiwa ni kwa maslahi ya WASOMALI au watu wengine waroho na wasio na huruma ya masikini wa somali land!!!watu hawa wamuogope mungu,watu wanaoteseka sana na hali ilivyo sasa somalia hawana hatia hata kidogo,na wala hawafahamu lolote kuhusu serikali,na tena hawafahamu vita!!ANGALIA WATOTO WALE WANAKUFA KWA NJAA!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
Karibu kila kitu kimemalizika kwa Serikali ya Mpito ya Shirikisho ya Somalia. Viongozi wa dunia wameipa muda serikali ya Somalia kuanza uchaguzi tarehe 20 Agosti 2012. Hata hivyo, tutaona kile kitakachotokea mjini Mogadishu siku zijazo. Na kuhusu al-Shabaab, majeshi ya AMISOM yameshakiteketeza kikundi cha al-Shabaab, bado kumebakia ngome moja tu imara kutekwa ya Kismayo. Jirani yetu Kenya ilisema ndani ya wiki moja litakuwa ndani ya Kismayu, kwa hivyo jambo pekee ninaloweza kusema ni kutumai bora zaidi hapa ambapo ninatoka.
SIDHANI KAMA NI BUSARA KUUA WATU KAMA HIVYO. NINAJIULIZA MWENYEWE KWA NINI WAISLAMU WANATAKA KUUA WATU WASIO NA HATIA? WAO WANAMUABUDU NANI? JE, MUHAMMAD ALIWAAELEKEZA KUUA? NI AINA GANI YA DINI INAYORUHUSU KUUA? TAFADHALINI TUMECHOSHWA NA MAUAJI YA WATU WETU NA NYINYI MNAICHAFUA DINI YA KIISLAMU.
Inatia wasiwasi kweli. Mungu awaongoze njia iliyonyooka vijana hawa waliopotoshwa na kufanywa wajiingize katika matendo ya dhambi kwa jina la jihadi (vita vitakatifu)? Ndugu zangu, vita vitakatifu vina masharti yake ambapo vinaweza kupiganwa. Muogopeni Mungu wenu na mtubu kwa vile toba inakubalika. Kama kweli mnataka kupigana vita vitakatifu, subirini kwani Mungu ataleta vita vitakatifu vya haki na acheni kuua watu wenu. Watu hao waliotangaza vita vitakatifu kwa maslahi yao wenyewe na kuwaambia vijana wawe wauwaji wa mabomu ya kujitoa muhanga au kupigana kwa jina la Mungu, mmoja wao akiwa mtu anayejulikana kama Hassan Hussein, hawakuwahi kuonekana hata mara moja akipigana kwa kile wanachokiita vita vitakatifu na waliobakia ni sawa na yeye. Hakuna yeyote kati ya hao wanaojiita viongozi aliyetekeleza uuaji wa bomu la kujitoa muhanga. Kwa nini badala ya kuwapotoa vijana, hawashiriki wao katika kujitoa muhanga kwa mabomu kama ni kweli watazawadiwa pepo? Muogopeni Mungu wenu, ndugu zangu.
Ripoti hii sio ya kweli. Yule aliyeiandika na watu wanaoiunga mkono wote ni wamoja.
HUKUMU ILIPITISHWA KWA AL-SHABAAB WOTE SIKU WALIPOUA BINADAMU WA MWANZO ASIYE NA HATIA, IWE MUISLAMU, MKRISTO, KAFIRI AU MWENGINE YOYOTE. WATAKUWA WAO WA KUPIGWA RISASI YA MWISHO IJAPOKUWA WENYEWE KWA WENYEWE WAKATI MTU WA MWISHO ATAKAPOKAMATWA NA KUSEMA WALITOKEA WAPI. SOMALIA ITAKUWA HURU. SOMALIA ITAFANIKIWA.
Hongera kwa K.D.F. Tunaelewa kuwa al-Shabaab ni waoga na watu wanaoangalia maslahi yao na tumefurahi kwamba kikundi hiki sasa kinavunjika… Tunatarajia amani kubwa.
Lini watu wa Somalia watafaidika na dakika moja ya utulivu? Upotelee mbali uoga wa Marekani na Waislamu wenye siasa kali waliopotoshwa. Wanaishi kwa kupigana na wanaowaona tu ambao daima wanapiga mikono chini katika makutano yoyote?
Sisi Wakenya tunajua tunachokifanya kuwatoa Al-Shabaab ndani ya nchi yao. Inasemekana ikiwa diplomasia inashindwa, nguvu itatumika. Askari wa Kenya endeleeni hivyo hivyo.....mpaka watakapopotea.
Al-shabaab wanatakiwa kufutika kwenye uso wa dunia
Matatizo ni Wamarekani walioingilia baina ya Kenya na Somalia ambayo ilikuwa ni kazi ya ndani kama ile iliyotokea katika World Centre ambako Wayahudi na Wamarekani walihusika na milipuko ambayo iliufanya ulimwengu uamini kuwa yalikuwa ni mashambulizi ya kigaidi. Watakuja na kila aina ya mbinu za kibinadamu lakini siku moja watakuja kulipa.
Mungu ndiye pekee aliyeumba na anayechukua maisha yetu.
Hongera KDF...Siku zote tunawaoombeeni. Zidisheni vita mpaka wote (al-Shabaab) watakapo sagwasagwa!!!!!!!!!
Kuna watu wengi katika kikundi cha al-Shabaab waliojitoa na kujiunga na vikosi vya serikali, na kujitoa huku ni ishara muhimu ya kuwepo kwa haki kwa machafuko na mgawanyiko ndani ya kikundi. Kujitoa huku ndani ya kikundi cha al-Shabaab karibuni kumetokea katika njia mbaya kutokana na mafanikio ya vikosi vya Umoja wa Afrika katika kudhibiti miji ya kimkakati nchini, ambayo ilikuwa inadhibitiwa na kikundi, na ambayo imejitenga na viunga vya mji mkuu wa Somalia, Mogadishu. Mwisho wa al-Shabaab uko karibu, kwa vile imekabiliwa na upotevu mkubwa katika kipindi kilichopita.
Kwa mawazo yangu, naamini uongozi wa nchi hii lazima upewe kikundi chochote ambacho kinaweza kuwasaidia watu, iwe al-Shabaab au serikali ya mpito ya shirikisho, lakini tunapendelea kikundi ambacho kitatawala kwa kutumia sheria ya Kiislamu kwa vile sisi ni Waislamu.
Vita gani hivyi vitakatifu? Kama wao ni wanaume wa kutosha, basi wajitokeze hadharani.
Mnaota, hamtawashinda al-Shabaab. Mtakufa nyote kwani wao ni jeshi la Mungu, Mungu akipenda watawasaga. Niko katika wilaya ya Kerugoya nchini Kenya.
Hongera kwa KDF, Amerika na nguvu zote zinazowapiga NGURUWE hawa WAPUUZI,WASO FADHILA..N.K..!
Wote al-Shabaab na wafuasi wao nchini Kenya na popote pale ni WAPUUZI. Ningekuwa rais wa nchi hii, ningekuwa nimeshawatokomeza wote kwa sababu ni watu hao hao ambao wanafanya mashambulizi haya ya mabomu nchini hasa makanisani. Kwa nini wasiende kuwashambulia Waislamu wenzao misikitini?..
Kwanza inatakiwa ijulikane hawa Al Shaabab wantoa wapi hizi silaha nzitonzito na inafanyika hivyo kwa maslahi ya nani? mimi siamini kama kuuwa watu kwa migongo ya dini ni kwenda mbinguni au kuepuka hukumu kali siku ya mwisho. Al Shaabab ni kundi tishio sana na halitakiwa hapa duniani!!
Iwe kulikuwa na dhuluma ya kihistoria iliyofanywa kwa mtu yeyote ikiwa ni pamoja na wale masheikh haiwapi nafasi wa kuua wananchi wasio na hatia. Tumekwenda mbali katika eneo lao na tutaweza kwenda mbali zaidi ikiwa tu mlingano utakuwa na uwiano. Hata hivyo, serikali na mataifa ambayo yamekuja kusaidia Wasomalia lazima wafanye hivyo kwa mioyo safi na sio kwa matakwa ya kichoyo. Wawe al-Shabaab au raia wema, wote wana haki ya kuishi!
Mimi skielewi hiki kikundi kwa nini iwauwe wanachama wake hadharani? Ikiwa ni hukumu ya kijeshi si wangechinjana huko kambini kwao badala ya kuwaaaninka hadharani? This scaring even to normal wananchi Somalis
Hawa ni waoga wanaojificha nyuma ya dini ili kumwaga damu.
Al-Shabaab na imani zao za kipuuzi wako nyuma kiteknolojia. Badala yake wanatakiwa kuendelea kila wakati teknolojia inapoendelea. Kama msemo unavyosema, "Kama msemo unavyosema "kama utaanguka kikamilifu utakuwa mpumbavu". Vijana wale wenye tamaa lazima wafunzwe tabia njema ya kutoendeshwa na mapenzi ya fedha bali waendeshwe na sifa za kibinadamu. Wanapaswa kutofuata viongozi wao kwa upofu kwa kumwaga damu ya binadamu ovyo....
Hao majamaa WATAANGAMIA kabisa!!!!!!!
Umasikini na njaa ambavyo Somalia inatesekea navyo kutokana na vikundi vya ugaidi ambavyo vimeiba kila kitu nchini, ikiwa ni pamoja na msaada na ruzuku zinazotolewa kwa Somalia. Vikundi vimeiba hivyo ili kuongeza mateso ya wananchi wasio na hatia ambao wamevumilia sana kwa sababu ya kuwepo kwao. Ni lazima kuvizuia vikundi hivi, na kuzuia vitendo vyao dhidi ya wananchi. Ni mara ngapi vikundi vimepigana wenyewe kwa wenyewe, na kusababisha kuanguka kwa wahanga wengi wakati wa mashambulizi yao? Ilikuwa ni lazima kwamba vikosi vya usalama kupambana navyo tangu mapema vikundi hivi, kwa sababu mashambulizi wanayolenga dhidi ya wanajeshi na kuua watu wake. Vikundi hivi vya kigaidi vimechafua sura ya Somalia ulimwenguni. Zaidi ya hayo, wanaifanya Somalia itengwe na dunia yote. Lakini, mpango wao huu haukufanikiwa na vikosi vya usalama vimeweza kukabiliana nao, kwa kushirikiana na mifumo mengine ya usalama.
ikopoa
alshabab kamwe hawata shinda ni ujinga tu wakuto elewa imani na kudanganywa na waarab!! stupid!!
Siku zao zinahesabika. Mungu mwenye uwezo mkubwa ulimwenguni atawasaga mmoja mmoja.
Mungu atawalaani na katu hawatakuwa kama walivyokuwa. Hawawezi kuendelea kuua watu wwa Mungu kama wanavyofanya. Hili lazima lisitishwe, kwa Mungu wa Mbinguni! Ikiwa wao ni Ibilisi na wanatafuta damu, waende kuua wanyama kama ni lazima kuua viumbe hai.
Ikiwa wanaamini katika vita, kwa nini wanawaua majasusi? Inaelekea kama kitengo chao cha intelijensia ni dhaifu na kuwaua ndio chaguo lao. Kwa vyovyote vile, Mungu yupo kwa kuiokoa hali hii, Amin, Amin.
Ikiwa wanaamini katika vita,kwa nini wanawaua majasusi? Inaelekea kama kitengo chao cha intelijensia ni dhaifu na kuwaua ndio chaguo lao. Vyovyote vile, Mungu yupo hapo kuiokoa hali hii, Amin, Amin.
kila kitu kina mwisho kama osama ameshindwa hata wao watashindwa,marekani na mataiifa mengine yasaidie na ziongeze wapelelezi wa kutosha na wawawezeshe mawasiliano yenye nguvu na masafa marefu bila mitambo ya al shababi kunasa.vile vile serikali ya sudani iunge mkono hadi mwisho.
Naamini Mungu amekuja kuikomboa Somalia kutoka mikononi mwa washirika hawa wa Shetani ambao wameinakamisha nchi na kuua watu wasio na hatia. Hebu dunia yote isimame na kuiokoa Somalia.
Kimbieni al-Shabaab...Kimbieni!
Idumu al-Shabaab, magaidi nambari 1 wa ulimwengu? Ninawapenda kwa sababu wanawafanyia ugaidi magaidi wakuu ambao ni Wakristo... kwa mfano Marekani, Uingereza, Ethiopia na Kenya pia.
hiyo ni laana tosha kwa Alsabaab kwani mwisho wao wakutawala umefika kwa hiyo watamalizana wenyewe kwa wenyewe kwani mtenda dhambi hujilaani mwenyewe kwanza mfijana wenyewe wanaoshiriki hiyo vita niwadogo kiasi kwamba hawawezi kuhimili vita visivyo kuwa na mwisho ndio maana wanataka kutoa siri ya viongozi wao marekani big up
ILA MI NAAMINI NJIA BORA SI YA KUUANA.ILI WATU WANATOFAUTIANA.NI SAWA NA KUSEMW UNAMUUA MGONJWA WA UKUIMWI ILI ASIENDELEE KUAMBUKIZA.ILA HUKUMU YA MUNGU NI YA MWISHO..SI SOLUTION
Wananchi wa Somalia wameshateseka sana kutokana na ugaidi. Hizi harakati zina dhamiri ya kuyumbisha usalama wa Wasomali na kufifisha hatima yao. Magaidi wengi wamefanya uhalifu mbaya sana ili kukamata udhibiti wa sehemu nyingi za Somalia; hasa kwa sababu Somalia haina mfumo imara wa usalama. Hii imerahisisha kuenea kwa vikundi vya magaidi nchini Somalia na kuigeuza nchi kuwa uwanja wa vita baina ya wananchi wasio na nguvu na harakati za magaidi na kusababisha fujo nchini Somalia. Nchi hii iliyo nzuri imekumbwa na njaa na uchumi mbaya sana. Umasikini na njaa vimeivamia Somalia, kwa sababu harakati hizi zimekuwa zikiiba misaada inayoingia katika ardhi ya Somalia kabla ya kuifikia serikali. Hili linafanya hali kuwa mbaya zaidi ndani ya ardhi ya Somalia.
Wengi wa wachangiaji hawajui historia ya wanachokieleza.Somalia ilikuwa imetulia chini ya Mamlaka ya Kiislamu na wasomali walikuwa wanaishi kama ndugu.Kwavile Marekani ni adui mkubwa wa Uislamu akachokonoa mambo na hatimaye alichokitaka ndicho kinachoigharimu Somalia mpaka sasa.Kaiondoa serikali halali ya kiislamu na kuweka mapandikizi ambayo yameshindwa kuendesha nchi na mpaka sasa hakuna dalili za amani,Insha allah !Mungu mkubwa siku moja amani itarejea kwa uwezo wake yeye na wala sio Marekani wala Mapandikizi yake
Ikiwa waoga hawa wanamwamini Mungu kwa nini basi wanawaua watu wasio na hatia katika kanisa nchini kenya, kwa mfano walirusha maguruneti ndani ya kanisa na kuwauwa waumini na kuwajeruhi wengine. Ikiwa wana matatizo na serikali ya Kenya ambayo inaongoza OPERESHENI LINDA NCHI nchi Somalia, basi watoe malalamiko yao kwa njia nyengine lakini sio kulenga dini. Wakristo na Waislamu wamekuwa wakiishi pamoja kwa miaka mingi na wataendelea hivyo kwa karne nyingi zijazo. Kenya sio taifa lililoshindwa kama Somalia na KDF litawasafisha na kuwatoa wote. Waendelelee kuwaua watu wengine lakini wasiwaletee Wakenya UPUUZI WA JIHADI….
Ni vizuri kusikia habari hii
tunashukuru kwa hilo..........
Ni upuuzi kufata imani isiyokuwa na taswira, yoyote yule amwagaye damu ya bin adam mwenzake lazima ajue kuwa ni mfuasi wa shetani na sio Allah, na waumini wa kikundi au dini yoyote inayoamini kwa kuuwa bin adam wenzake eti watapata thawabu kwa mwenyezi Mungu ni upuuzi mtupu, God is not stupid like that. Damu waliyoimwaga itawalilia na kuwamaliza wenyewe kwa wenyewe na kizazi kwa kizazi, na pia wakazi wawapuuze kwa kutokwenda kushuhudia mauaji hayo ya kinyama
Aluta Qontinua
Sijawahi kuzungumza nyuma ya simba ninayemuona.
Al-Shabaab ni wavunjaji wa haki za binadamu.
ukiua kwa upanga nawe utauwawa kwa upanga na ndicho kinachotokea sasa kwa hao magaidi mungu sasa anawaadhibu
Al-Shabaab kimeundwa na watu ambao ni wapigananji wa vita vitakatifu na wanapigana na maadui wa Mungu na wale wanaoipiga vita dini ya Kiislamu na mtawaona wakiitawala Somalia yote, Mungu akipenda.
Al-Shabaab yenyewe imeandikisha watu kwa kutoa fedha kwa vijana. Uongozi wake usilalamike pale ambapo zawadi ya dola milioni 33 imewekwa juu ya vichwa vyao.
kila ovu lina mwisho wake, naamin mkonno wa mungu unafanyakazi
Wote watakufa vifo vyenye uchungu.
Nadhani hiyo itakuwa ya kipekee kabisa
ALSHABAB NI WAKALA WA SHETANI
alshabab nawaomba muwe watuliv katika nchi yenu kwasabab hamuna mtu atakaye kuja huko somalia kuleta aman ni ninyi mtakaye hakikisha amani inakuwapo huko somalia, pia hao vibaraka wa kimarekani na uingeza wao hawana nia ya kuleta amani bali machafuko, nia yao kubwa ni kuhakikisha amani afrika inatoweka kabisa. ninachoshauli ni kwamba afrika tuwe na umoja wa kutafuta suluhisho sisi wenyewe.
Kinacho waua wasomali mpaka leo hii ni damu ya (mashekhe) waliochinjwa kama mbuzi hapo nyuma. Hivyo, suluhisho la matatizo ya somalia ni kuruhusiwa kuwa chini ya serikali ya kiislamu kama ilivyokua awali, mbali nahivyo mapigano yataendelea mpaka Qiyama.
Mwenyezi mungu hakutoa haki kwa binadamu kumuua mwenzie, ni yeye tu mwenye kufanya hivyo kwa namna anavyotaka kumuadhibu mtu ambaye anamkosea, Hivi hawa Al-Shaabab wamepata wapi amri ya kuua watu wasio na kosa/hatia mbele ya haki? Dhambi zao zinawarudia na wataagamizana wao kwa wao kwa sababu wote ni wauaji na mungu hataki kiumbe chake alichokiumba kihukumiwe na mwanadamu mwenzie, hiyo ni raana ya mwenyezi mungu
Hakuna ubaya unaoweza kuepuka adhabu! Utukufu uwe kwa Mungu!
Hivo ndivyo njia inavyotakiwa, lazima al-Shabab ijue kwamba huu ni wakati wao wa kuondoka.
Poleni sana ,kuna ndugu zenu wanateseka sana huko msumbiji, wanaishi kama wanyama sababu kukimbia hiyo vita. malizeni vita ndugu zenu walejee kwao,
Walio katika njia sahihi watashinda. Allah huwalinda na kuwarehemu waja wake kwa nguvu yote na kwamba hakuna mwenye ubavu wa kuzuia.
Alshabab bado wana nguvu na watashinda kwani ninavyoamini katika vita yoyote kuna kushindwa halafu baadaye mapambano yanaendelea, kwa hiyo hao vibaraka wa mmarekani na uingereza wajue watapata shida baadaye.
Matayo 10:28 Msiwaogope wale wauao mwili, lakini hawawezi kuiua roho. Badala yake, kuwa na hofu na yule awezaye kuangamiza mwili na roho katika moto wa Jehanamu. Waebrania 10:31 Ni jambo la kuogopa kuanguka katika mikono ya Mungu aliye hai.
Al-Shabaab ni zao la ujinga wa Waislamu wengi na hawawezi kuushinda uhuru, wengi wa watu hawa wanatoka Somaliland.
Aibu kwa wanaowaunga mkono na kuwapatia fedha al-Shabaab, wanaofikiria kuwa wanamtumikia Mungu kwa vitendo vya kishetani. Mungu wao ni dhaifu, anahitaji ulinzi wa binadamu.
inapendeza mnavyotupa habari kama hizi endeleeni kutuletea na nyingine zenye uchambuzi wa kina
Al-Shabaab ilikuwa inajulikana tangu mwanzo kwa kutoijali Somalia na wanachama wake karibu wote walikuwa wageni wenye itikadi potofu ya vita vitakatifu akilini mwao lakini wengi wao sasa wameijua al-Shabaab, isipokuwa wachache tu ambao watajua karibuni.
Ni nzuri, kuwa fisi ameanza kula utumbo wake mwenyewe. Ahadi ya kutoa zawadi nono kwa vichwa vyao inafanya maajabu kwa vile wengi wao wanahamasishwa na pesa, na sio itikadi. Itakuwa nafuu kubwa sana (hasa kwa Wasomali) wakati kikundi cha al-Shabaab kitakapomalizwa daima.
Al-Shabaab wanakuwa dhaifu kama jua linalotua lakini tahadharini na wale Wasomali walio na maslahi mamoja wakati fulani watapigana wenyewe kwa wenyewe baada ya al-Shabaab kutokomezwa kwa sababu lengo lililowaunganisha lilikuwa kupambana na al-Shabaab. Kuweni na tahadhari juu ya ukweli huo na mlitie akilini.
Inaeleweka kwamba watu sio waaminifu wa dini wanayodai kuilinda kwa hivyo kuitumia ili kukidhi maslahi yao ya kichoyo kwa kuwapotoa wengine kwa itikadi zao potofu. Hili linanisikitisha sana. Ningependa kuwaomba Wasomali kuasi waziwazi dhidi ya watu wanaoua wengine bila ya sababu yoyote wakati wote.
Kwa kuwa Mungu anawapenda watu wake waacheni waadhibiwe mara mbili kwa sababu walimfanyia makosa. Ni wakati wao sasa wa kuteseka kama ambavyo wamekuwa wakiwaangamiza na kuwaua watu wasio na hatia.
Big up mwandishi wa makala hii, unatuhabarisha mambo muhimu
Tukitaka tuinusuru Somalia basi ni lazima turejee nyuma kidogo,Siadbare alifanya makosa ambayo hadi sasa yanaizuru Somalia, lakini inawezekana kabisa, unajua Wasomali ni Waislam na waislam si wakaidi basi ni bora Somalia ipewe mamlaka kama ilivyokuwa pale mwanzo, ikiongozwa kwa sharia hii ndio (solution)
Kilicho na mwanzo hakikosi mwisho. Mungu yupamoja na wasomali wapenda haki.
Sawa.
Nina imani na serikali ya mpito ya shirikisho.
Dua zangu ni kuwa siku moja wanawake, watoto na wanaume wa Somalia waishi kwa amani kama mtu yeyote duniani. Al-Shabaab lazima waondoke sasa. Asanteni Jeshi la Ulinzi la Kenya, askari shujaa wa TFG na AMISOM.
Naamini ikiwa serikali ya shirikisho ya mpito iko sahihi, itafanikiwa kwa kupata imani ya wananchi.
ni bora wasomalia woote wakaungana na kupigania nchi yao maana ni bora muwe na umoja wa nchi maana wanaoteseka ni wao na hasa watoto na wanawake nawashauri wasiikimbie nchi yao wakae wapambane
tatizo la makundi ya kigaidi ni kutoaminiana na kwakuwa wanachokifanya ni dhambi mwisho wa siku huukizana wenyewe kwa wenyewe'na hapo ndo kusambaratika kunapokuja na mwisho wa magenge ya waovu hao ndo unafika,nai-penda.
Nimefurahi kuwa hili ni mwanzo wa njia kuelekea dunia iliyo salama zaidi. Ninaunga mkono juhudi za kupunguza uwepo wa kikundi hiki cha kigaidi ambacho kimesabababisha maangamizi na woga kwa watu wote duniani.
HATIMAYE WATASHINDWA
iko poa!
Ni wazi sasa kwetu sote kuwa watu hawa wenye imani dhaifu wanasema kwaheri kwa kuuwana mmoja wao. Dunia ina kila sababu ya kutabasamu juu ya hili. Tuombe sana kwa ajili yao kwa kumaliza vizuri na si iliyo mbaya.
Tunaishurkuru dunia yote kwa kukubali kuingilia kati Somalia hasa Wamarekani ambao daima huwepo pale amani inapopiganiwa. Mungu ibariki Marekani.
Shukrani kwa jeshi la Uganda. Lilikuwa la kwanza kupeleka jeshi lake kule. Watawaondoa waoga hao.
alshabab wanapowauwa wanachama namnahiyo wanategemea wakati wa uchaguzi ninani atawapigia kura wagombea maana wananchi ndio hawo wanaisha
Vyenye nataka kiwango cha kuaminiana kishuke ili kikundi cha wanamgambo kidhoofike.
Hongera intelijensia ya Kenya kwa kuwatoa nje wanaharamu hawa….Nchi nyenye nguvu ya Afrika ya Mashariki.
Al-Shabaab ni harakati iliyotumwa na Mungu kuwaadhibu Wasomali baada ya kutupa serikali yao na kuwa na tabia kama ya wanyama. Namuomba Mungu atulinde kutokana na vikundi vinavyoleta shida hii chini ya jina ya dini. Wakati wao wa kuvunjika umefika.
Somalia itanawiri tena na kuongozwa vizuri. Hilo ndio tunalotegemea. Al-Shabaab kwa sasa wanakaribia mwisho wao. Ubaya haujawahi kuushinda wema. Muda wote ambapo Mungu yuko katika kiti chake.
makala makini sana
Wameua watu wengi wasio na hatia na sasa wanageukiana wao kwa wao. Hatimaye wote watajiua wenyewe. Hii inadhihirisha kuwa hawana dhamiri yoyote wanayoipigania.
Al-Shabaab lazima watolewe na vikosi vya AMISOM. Kikundi hiki kimewatesa na kuwaua watu wengi nchini Somalia. Nchi imeharibiwa kabisa ambapo itaichukua serikali ya Somalia muda mkubwa kuiimarisha. Wengine duniani wanaombwa kusaidia katika kuijenga upya Somalia wakati vita vitakapomalizika. Serikali ya kenya imeisaidia sana Somalia katika vita ili kuing’oa al-Shabaab na tunaishukuru Kenya kwa juhudi walizojitolea kuokoa maisha ya watu wa Somalia. Pamoja na hayo, Kenya isaidie kwa njia zote kwenye vita vya Somalia na maisha ya watu kwa vile sasa AMISOM inakaribia Kismayu kuwang’oa al-Shabaab nchini. Afrika inapaswa kuungana na kuibuka pamoja kusaidia kuwatoa al-Shabaab kwa namna yoyote ile. Tunataka watu wa Somalia waishi katika amani na kuendeleza nchi yao ambayo imekwama kwa muda wa miaka 24 sasa.
Nayapenda sana.
Nadhani kudhoofika kwa uaminifu baina ya vikundi vya al-Shabaab ni habari nzuri sana kwa Msomali yeyote ulimwenguni. Hongera nyingi kwa Wasomali na Wasomaliland na kwa heri al-Shabaab, mpo kwenye hatua zenu za mwisho!!!
Ni mara ya mwanzo kujifunza au kukishambulia kikundi hiki kwa kusema kitu kuhusu wao na kunao matatizo mengine mengi yanayoikabili kikundi hiki ndani ya wao wenyewe au kutoka kwa watu.
Naamini kuwa Serikali ya Mpito ya Shirikisho iko sahihi, itafanikiwa kwa kupata imani ya wananchi na itapata uwezo wa kuwashinda maadui kupitia njia zifuatazo: 1. Watu kuiunga mkono. 2. Eneo la kijiografia ambapo ipo. 3. Imani ya kufa kwa kile inachopigania.