Julai 23, 2012
Jeshi la Somalia, likiungwa mkono na vikosi vya Misheni ya Umoja wa Afrika Somali (AMISOM), vinajiweka sawa kuichukua miji na vijiji huko Juba ya Chini vikisonga mbele kuelekea mji wa kimkakati na ngome kuu ya al-Shabaab huko Kismayo.
Meja Jenerali Abdikarim Yusuf Dhegobadan alisema anatarajia majeshi yake kuisafisha Kismayo, mji mkuu wa tatu kwa ukubwa wa Somalia ulioko kilomita 500 kusini ya Mogadishu, wa al-Shabaab ifikapo mwezi Agosti .
Dhegobadan aliiambia Sabahi kuwa magaidi wamekuwa wakikimbia kutoka mafichoni mwao huku majeshi ya Somalia yanasonga mbele.
Alitoa wito kwa wakazi kuhama maeneo yalipo chini ya udhibiti wa al-Shabaab na kuondoka kabisa kutoka maeneo yenye maficho ya silaha.
"Kismayo ni ishara kwa Serikali ya Mpito ya Shirikisho ya Somalia (TFG), na ndio maana inajaribu kuuchukua mji huo," alisema.
Kwa mujibu wa mbunge Mohamed Omar Gedi, siasa kali za al-Shabaab na uhalifu dhidi ya binadamu, ambao ni pamoja na uuaji wa wanazuoni wa Kiislamu, wasomi na yeyote anayepingana nao, umepitiliza sana.
Gedi alisema jeshi la Somalia karibuni litawapondaponda magaidi na kwamba washirika wa al-Qaeda, al-Shabaab, wako katika saa ya kifo.
"Vikosi vyetu vimepiga hatua katika mapambano ya mwisho na viongozi wa wakuu na wanamgambo wao wamejawa na hofu," aliiambia Sabahi. "Tutachukua udhibiti wa Kismayo wakati mapigano mapya yatakapoanza na moto wa risasi kuwazunguka [maadui]. Tutashinda na amani itapatikana."
Maafisa wa kijeshi wa Somalia walisema operesheni za kijeshi zinategemewa kuenea hadi Juba ya Chini baada ya TFG kuwa kuwaandaa wanajeshi wake kuelekea Marka, mji mkuu wa Shabelle ya Chini na Jowhar, mji mkuu wa Shabelle ya Kati .
Naibu Waziri wa Usafiri wa Anga, Bahari, Ardhini na Bandari Abdirahman Kulmiye Hirsi alisema kuwa kukamatwa kwa Kismayo, ngome kuu ya al-Shabaab iliyobakia, kutakuwa pigo la mwisho kwa kikundi.
"Vikosi vyetu vitazidisha kampeni za usalama na mashambulizi kuyalenga makambi ya vikundi hivi katika maeneo kadhaa kwenye mikoa ya Gedo, Shabelle ya Chini, Shabelle ya Kati na Juba ya Chini ili kulinda bandari, viwanja vya ndege na barabara na kuruhusu upokeaji wa misaada na usaidizi wa afya kwa watu walioathirika kwa matumbo ya kuharisha na kipindupindu , ambayo hivi karibuni yamekuwa maradhi," aliiambia Sabahi.
Msemaji wa zamani wa AMISOM Meja Paddy Akunda alielezea mpango kabambe wa kuitekea Kismayo ili misaada iweze kusambazwa na wakazi kuweza kuendelea na maisha ya kawaida.
Akunda aliwaambia waandishi wa habari mjini Mogadishu kuwa watu karibuni watapokea habari njema kuhusu Kismayo.
Wakazi wa Kismayo wanasema wanasumbuliwa na matatizo ya kifedha, uhaba wa maji, kukatikwa kwa umeme, upungufu wa chakula na madawa kutokana na al-Shabaab kuukamata mji huo, na huishi kwa uoga kwamba kikundi kitafanya mashambulizi ya kulipiza kisasi wakati majeshi ya Somalia na AMISOM yatakapokaribia.
Anab Mohamed Musa, mwenye umri wa miaka 36, alisema alikimbia Kismayo miaka mitano iliyopita baada ya al-Shabaab kumzuia kuuza miraa, ambayo ni halali nchini Somalia, ili kuwalea watoto wake watatu.
"Madaktari, wafanyakazi wa misaada, waandishi wa habari na hata wanafunzi wengi waliosoma Kiiingereza mjini walishutumiwa kuwa wanafanya upelelezi kwa mashirika ya kiintelijensia ya Magharibi, hivyo iliwabidi kukimbia," aliiambia Sabahi. "Kikundi cha waasi kilisimamia simu za mikononi kupitia makampuni ya mawasiliano ya wenyeji ili waweze kusikiliza mazungumzo na kuendesha mauaji na kuzuia mipango dhidi ya kikundi."
Mkazi wa Kismayo Abbas Mohamed aliiambia Sabahi kuwa wapiganaji wa al-Shabaab waliwazuia idadi ya wananchi wazee wasisafiri kuelekea Mogadishu kupata matibabu muhimu kama sehemu ya juhudi za kikundi kuzuia wakazi wasikimbilie maeneo ychini ya udhibiti wa TFG.
Alisema pia al-Shabaab wanawasumbua wanawake, wakilazimisha kanuni kali za mavazi na kuwazuia wasifanye kazi.
Mohamed alisema al-Shabaab wanawalazimisha karibu wanaume wote wa Kismayo kubeba silaha na kuwapa mafunzo ya vita vya msituni, kulazimisha mtindo wao wa mavazi ili kusiwe na tofauti yoyote baina ya wananchi na wanamgambo.
Al-Shabaab pia wamewafunza wanawake na wasichana kufanya mashambulizi, alisema, na kwa muda wa miaka mitatu iliyopita, wamekuwa wakitoa zawadi za bunduki aina ya Kalashnikov na mabomu ya kurusha kwa mkono kwa wanafunzi wanaohifadhi Koran.
Mohamed alisema watu wamekuwa wakichukia tabia za al-Shabaab na uchokozi wao.
"Wanamgambo wa kikundi chenye mafungamano na al-Qaeda kilipanga na kutekeleza matendo ya kutisha ambayo yanauaibisha ubinadamu, kama vile kumpiga kwa mawe msichana hadi kufa kwa uzinifu, ambapo hajabaleghe bado," akisema. "Hili lilifanyika bila ya hata kuendesha uchunguzi wa kina wa makosa [dhidi yake] na bila kufanyiwa vipimo vya kiafya ili kuthibitisha uzima wa akili na mwili wake."
Ujumbe kutoka Jumuiya ya Maendeleo ya Pembe ya Afrika (IGAD) uliwatembelea maafisa mjini Mogadish...
Mshukiwa wa ugaidi na mke wake walipigwa risasi na kufa na maafisa sita wa polisi walijeruhiwa wa...
Watu watano walikamatwa siku ya Jumanne mjini Dar es Salaam wakiwa na vifaa vya kulipua katika mi...
Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta aliwataka wabunge kuweka kando madai yao ya kuongezwa mishahara kwa ...
Majeshi ya serikali ya Somalia waliwaua wanamgambo tisa wa al-Shabaab wakati wa mapambanao hapo J...
Mtu asiyejulikana alimpiga kwa risasi na kumuua ofisa wa kitengo cha usalama cha kijeshi huko kas...
Muungano wa Jubilee tawala cha Kenya kilichukua uongozi wa kamati mbili muhimu za bunge Ijumaa (t...
Chama cha Wafanyabiashara na Asasi ya Chakula na Kilimo ya Umoja wa Mataifa vinatoa mafunzo kwa w...
Balozi wa Umoja wa nchi za Ulaya nchini Tanzania Filiberto Ceriani Sebregondi aliwahamiza waandis...
Makamu wa Rais wa Kenya, William Ruto, alisema kazi za Misheni ya Umoja wa Afrika nchini Somalia ...
(Sera za kutoa Maoni) *Inaonesha Maeneo yanayohitaji
Maoni ya msomaji
Ni wazi sasa kuwa al-Shabaab imeshindwa na hii imekuwa ni kutokana na juhudi ya watu wa Somalia pamoja na vikosi. Kwa kuwa baada ya kushindwa maisha yanarejea taratibu katika hali ya kawaida na watu wanashughulikia kuijenga upya nchi yao- Serikali pia inaimairisha usalama.
Al-Shabaab inajukikana duniani kote kama kikundi katili kabisa ndani ya Afrika ya Mashariki na Afrika kwa jumla. Kikundi hiki cha kigaidi kimesababisha matendo yasiyosemeka ya kikatili na uvunjaji wa haki zabiandamu. Wale waliokuwa hawakubaliani nao waliadhibiwa vikali ama kwa kifo au kukatwakatwa sehemu za miili yao. Kikundi hiki cha ugaidi kimechukuwa dhamana wa upigaji mabomu na mauaji ya kujitoa muhanga nchini Somalia na nchi jirani. Watoto wadogo walitekwa, kuteswa na kugeuza kuwa askari bila aina yoyote ya mafunzo; hii ilipelekea wengi wao kuuwawa vitani na vikosi vya serikali. Al-Shabaab pia wamekuwa dhamana wa ugaidi katika bahari kuu na kuathiri biashara ya kimataifa pamoja na utalii wa Afrika ya Mashariki. Watu wengi wa Somalia wameteseka sana na wamekuwa hawajajua amani kwa muda mrefu; wamegeuzwa kuwa wakimbizi wakilazimika kuvumilia njaa na magonjwa.
Mwenyezi Mungu awalindeni nyote wakati mnaendelea kufanikisha kazi hii ya heshima.
Tumeona mkono wa Mungu kwenu. Sasa shindeni na shindeni na shindeni. Tunawaungeni mkono KDF kwa sala zetu. Tunawatakieni mafanikio.
Tunaomba kwa KDF na TFG na yeyote mwanye dhamira njema kwa Wasomali, kushinda vita hivi ili kuleta amani nchini na duniani kwa jumla.
Walinde amani kwa ajili ya kaka na dada zetu, wameteseka kwa miaka mingi.
Nzuri sana, ni furaha kwa Wakenya kuona majirani zetu wanaishi kwa amani.
Kutekwa kwa Kismayu kumechelewa sana. Msimamo mkali lazima utokomezwe na daima usiruhusiwe kustawi popote ulimwenguni.
Huu ni wakati wa kumaliza tishio la lililokithiri muda mrefu la al-Shabaab ambalo limefanya uhalifu dhidi ya binadamu kwa jina la Mwenyezi Mungu. TFG na KDF endeleeni kwa ujasiri na kumaliza misheni hii; watu wa Somalia wameshateseka vya kutosha.
Tatizo ni kuwa mkaidi. Mungu akusaidie kumaliza tatizo hili ambalo lilikuwa linawaathiri Wasomali kwa robo karne.
Ninapenda na kutarajia tu kuwa siku moja nchi jirani zetu zitakuwa katika amani kutokana na tishio hili la kila mara kutokana na ugaidi na kwa hivyo kuweza kufaidi matunda ya nchi zao ambazo wamezipigania sio tu tangu miaka mingi nyuma bali kutokana na mashambulizi haya ya kigaidi dhidi ya watu wasio na hatia. Amani ya Bwana wetu iwe pamoja nanyi.
Ninamuomba Mungu awasamehe kwa maovu wanayofanya na awabariki KDF kwa kazi yao ya kuuteka upya Kismayu. Asante.
Si hiari ya watu wa Somalia kuwa wateseke lakini walijikutia katika mapigano, lakini ni kwa sababu watu wachache wasioridhika wanaojiita al-Shabaab ambao hawana hatima kwa nchi yao achia mbali wao wenyewe. Wanapaswa kufahamu kuwa kadiri watakavyoacha mapema kupigana ndivyo itakuwa bora sio kwa wao tu bali kwa watoto wajukuu na vizazi vijavyo.
LAKINI WATU WANGU, WAKATI UTASEMA AMBAPO MTASIKIA KUWA WENGI WA ASKARI WETU WA KDF WAMESHINDWA KUTOKA NJE YA SOMALIA. NAAMINI BAADA YA MUDA BAADHI YA KDF WETU WATACHINJWA. TUSUBIRI.
Wasiwasi wangu mkubwa ni kwa vijana hawa juu ya imani yao ya Kiislamu dhidi ya kuua raia wasio na hatia.
Umeweka majenereta? Mimi niko huko kama fundi mitambo. Lol.
Tuko pamoja katika maombi. Mungu awajaalie ushindi na kuiteka Kismayu, mko huko ili kuwakomboa watu wake. Kumbukeni kuwa nyinyi ndio Musa wa leo. Natamani ningejiunga na kufanyakazi ya kutumia nguvu iliyoko mbele yenu lakini ninawaombea nyinyi na familia zenu.... malizeni misheni na mrejee nyumbani .... Hongera....
Msisahau kuwaambia juu ya Mungu na mtoto Wake, Yesu. Enezeni Neno la Mungu bila ya woga. Komboeni nafsi zenu pia, na hiyo ni misheni yenu vile vile.
Ewe Mungu! Wasaidie viumbe vyako vipendwa!
Mungu atawafanyieni njia KDF. ENDELEENI BILA KUCHOKA HAKUNA KURUDI NYUMA.
Endeleeni na moyo huo huo KDF na AMISOM kwa ajili ya misheni ya kuokoa maisha.
Matakwa yangu, Matumaini, Imani na Dua ni kuwa Mungu atawapeni hisani ya kuwateka na kuwasafisha al-Shabaab/al-Qaida kutoka eneo lote la Somalia mara moja na kwa matokeo mazuri, na Afrika itakuwa na ladha ya amani. Tuunganishe juhudi zetu na kuanza kusherehekea kwa vile naelewa Mungu ni mwaminifu, anachotaka pekee ni kwa sote kumuamini yeye. Amin. Amin.
Bwana wetu mwema awasaidieni nyinyi majamaa kushinda vita hii. Sio rahisi lakini Mungu akiwa pamoja nanyi mtashinda.
HONGERA KWA KDF, NENDENI, NENDENI MKAUTEKE MJI
MUNGU aonekane katika misheni hii ya kuwakomboa watu wa Somalia kutoka ukandamizaji.
Kazi nzuri imefanywa, lakini (AMISOM) usimamizi wa wakati wenu unasubiriwa Kismayu na wakaazi wa eneo lote kwa ajili ya uhuru.
Ikiwa shinikizo endelevu litawekwa kwa makabwela hawa, kikundi cha wanamgambo wa kupiga na kukimbia, bila ya shaka ushindi utapatikana kwa KDF na washirika wake na matokeo yake ni ukombozi kamili wa Somalia. Binadamu wa Somalia wanastahiki haki ya kuwa huru kama watu wengine popote pale duniani. Kitu muhimu kwa KDF na wengineo lazima wakumbuke kuwapa motisha wa kuwakomboa wale wanaokandamizwa. Zaidi ya hayo, tunawatakia askari wetu kila la heri.
Hatimaye tunapumua kwa sababu mashambulizi ya al-Shabaab yatakuwa historia.
Kumbukeni kuwa sio al-Shabaab wote, al-Qaida, KDF,UDF, TFG na kile mlichonacho, HAPANA bali ni mamlaka ya taifa la Somalia. Ndani ya Afrika yote, kwa nini nchi huangukia katika mtego wa vita vya wenyewe kwa wenyewe ni utawala mbaya, uchoyo na mtikisiko wa wakuu wa makabila ambao baadaye hugeuka Mabwana wa vita kwa jina la 'watu wangu', kwa hivyo, ili kujaribu kutatua matatizo ya majirani zetu lazima kwanza tuweke utaratibu katika nyumba zetu. ASKARI WA KENYA MKO KATIKA MIKONO YA MUNGU AMBAYE ATAWAZAWADIA KWA KUJITOLEA KWENU NA WAJIBU WENU KWA TAIFA LENU NA RAIS WA KENYA.
NDANI YA SIKU SABA, MJI WA JERICHO ULIHARIBIWA NA NDANI YA SIKU SABA MJI WA KISMAYU UTATEKWA NA TFG NA KDF, HONGERA! UHURU UPO KARIBU KWA WAKAAZI WA KISMAYU.
Ninahuzunishwa sana na watu wa Somalia ambao wamefanywa mateka na al-Shabaab na kulazimishwa kufanya yasiyofikirika!, lakini itafika siku ambapo Somalia itakombolewa. ENDELEENI AMISOM, NENDENI KISMAYU!
Katika maisha hakuna kitu muhimu sana kama unapoelewa kuwa ni wewe tu unayepaswa kumuauni binadamu wenzako wanaokandamizwa. Kwa hivyo HONGERA KDF HINGERA AMISOM, msiangalie nyuma mpaka mfike huko, nakusudia KismayO. Mungu ayasikie maombi yetu na kuwaokoeni na kila aina ya moto huko, Amin!
Sawa sawa. Amani inakuja nchini Somalia, Mungu akipenda.
Heko vikosi vya pamoja, tusafishe uuaji ndani ya Somalia, MUNGU yuko pamoja nanyi.
TUWAOMBEA NYINYI WATU, MNAFANYA KAZI NZURI
Wapanguzeni wote wenye akili za kishetani ili kusafishia njia mfumo mzuri wa maisha kwa jamii ya Somalia isiyo na hatia. Ni Mungu tu atakayelidhibti taifa zuri kama hili.
Hongera vikosi vya washirika.
Tunapaswa kueneza mwako wa fikra sahihi na mawazo ya dini kupitia elimu yenye ubora na vyombo vya habari vyenye uelewa, na kwa kutokomeza umasikini, ambao ndio sababu kubwa inayowapelekea watu kufuata itikadi kali. Watu hawa masikini wanajihisi kukandamizwa na kuchanganyakiwa. Lazima tutatue tatizo la ukosefu wa ajira, ambalo huwapelekea vijana kujisikia watupu, jambo linalosaidia kuleta mazingira yanayowafanya vijana washawishike na mawazo ya wanamgambo. Hili pia ni pahali jukumu la asasi za kidini linapoingia. Wanasaidia kueneza mfumo wa kuwaza kwa wastani, wanawaelimisha vijana kuhusu hatari ya kujishughulisha na fikra za siasa kali; wanasambaza utamaduni wa utofauti na ubadilishanaji mawazo kwa uhuru wa kusema na kupata uhuru wa umma na wanaanzisha mfumo wa maisha ya kidemokrasia katika jamii, kunakoruhusu uhuru zaidi unaoeneza mawazo ya kuvumiliana zaidi na kuwasaidia watu wawe wazi zaidi kwa wengine.
KDF wako wapi? kwa nini TFG wanataka kuiteka Kismayu sasa? Tusubiri tena mwaka mmoja au mlifanya hivyo? Nadhani mngewaachia KDF wapigane na muje baadaye kujiunga. Niko sahihi?
Wasafisheni wanamgambo hao na safisheni njia kwa utawala bora nchini Somalia...tufanye biashara pamoja (Kenya na Somalia).
Al-Shabaab wako njiani kutoweka. Watasahauliwa kabisa kama walivyosahauliwa Sadam Hussein, Osama bin Laden, Muammar Gadaffi na Hosni Mubarak.
Ijulikane kwamba JEHOVAH, YEYE NDIYE MUNGU. Shalom.
Bwana Jah, tafadhali irejeshe Somalia kama tulivyofanya Wakenya. Asante.
Ronald, wewe ni nani, Mkenya au al-Shabaab unayejificha?
Endeleeni kuwasha moto,... hongera KDF, kusiwe na huruma linapokuja suala la kupambana na maadui wa amani. MUNGU atawasaidieni kuwaokoa wananchi wasio na hatia wa ardhi ya Somalia.
Nadhani hawa al-Shabaab wamekuwa maumivu ya kichwa kwa KDF. LAKINI NILIDHANI kuwa hawa al-Shabaab huko Kismayu walikamatwa mwezi uliopita.
Nilidhani KDF ilitarajiwa kuiteka Kismayu mwaka jana, kilitokea nini? Sasa makala hii inatuaambia kuwa ni TFG itakayoiteka Kismayo. KDF kuweni wabunifu, tafadhalini.
Kwa kweli inauma sana kuona kikundi cha watu kuwaweka watu wengine kizuizini kwa sababu za uchoyo ambazo hazina maana kwa jina la Mwenyezi Mungu. Mungu mwenyewe ni upendo. Wamekuwa wakiwakandamiza watu wa Somalia kwa miongo mingi. “Ujinga umwatawala hawajui kuwa huu ni uovu,” sasa kwa vile wale waliokuwa wakikandamizwa wanapata nafuu wao wanafikiria kuwa hilo ni baya na wanataka waendelee kua watu wasio hatia. Tuwaombee wakombozi na tuwaombee watu wa Somalia. Amani itawale Afrika na Mungu ibariki Afrika.
Ni vizuri mumeondolewa nyinyi magaidi. MJAALIWE MUSAGWE KWA NGUVU NA VIKOSI VYA SERIKALI, ILI KUWEPO NA SHERIA NA KANUNI NCHINI SOMALIA.
Vizuri! Hadithi ya al-Shaabab itakuwa hadithi ya kuwasimulia kizazi kijacho na ni kweli kwamba jamii inakuwa kubwa pale wazee wanapopanda miti ambayo kivuli chake wanajua wazi hawatakikalia chini yake. Hongera KDF, UPDF na jeshi la Ethiopia ambao kwa moyo safi wanapanda miti ambayo pengine hawateza kupumzika kivulini pake lakini ni kwa faida za siku za mbele za wavulana na wasichana wa Somalia yenye amani tunayoitaka.
Ninawatakia kila la heri kwa vile wanadhamiria kuisafisha al-Shabaab. Tunatumai wanafanya vizuri sana.
Bila shaka wakenya tuko nyuma ya KDF.Kazeni kamba vivyo hivyo.
Hongera KDF; Bwana yuko pamoja nanyi. Mtashinda kwa niaba ya wananchi wanaoteseka wa Somalia. Wenye hekima wote wa dini ikiwa ni pamoja na Yesu Kristo (mwokozi wetu), Mitume wote ikiwa ni pamoja na Muhammad (Amani Iwe Juu yake) wangefurahia kazi yenu leo. Mnawakomboa watu wanaoteseka kutokana na watu wanaotumia dini ili kuwakandamiza. Tutawaombeeni mpaka mtakapoikomboa Kismayu na Somalia yote.
Bwana awe pamoja na timu ya AMISOM, na una moyo kwamba karibuni watahukumiwa.
NGUVU ZA MOTO WA KDF UENDELEZWE. ENDELEENI KDF, TUNAJUA KAZI HII SIO RAHISI LAKINI TUNAJUA PIA KUWA NYINYI MMEUMBWA KWA KWA AJILI YA KAZI HII KWA HIVYO HAKUNA KUANGALIA NYUMA. MUNGU AWE PAMOJA NANYI.
Kazi nzuri vijana, Mungu awabariki.
Kwa kweli ninaishukuru KDF na MUNGU awape NGUVU na UJASIRI, tuko pamoja katika maombi.
Bunduki za Kalashnikov haziwezi kuzuia mashambulizi ya anga na gari za KDF ambazo zinaweza kuhimili milipuko ya al-Shabaab. Isipokuwa ukosefu wa busara unapompata yeyote, kwa kweli sioni kwa nini kukiunga mkono kikundi hiki cha wanamgambo wapuuzi.
Tuna waomba muongeze kasi ya kuwadhibiti waasi hao.
Nadhani wakati KDF ilipoingia katika kuwasaka al-Shabaab ilionekana kama ndoto isiyowezekana, lakini kutokana na mtandao mzuri wa upelelezi na msaada kutoka kwa TFG na AMISOM, adui sasa anakimbia na muda mfupi itakuwa furaha huko Kismayu kwa vile mji huu utakuwa huru kutokana na tishio la al-Shabaab, ambao walikuwa wameuteka nyara kwa muda mrefu. Zaidi ya hayo, ninawatakia kila la heri na Mungu awalinde.
Mungu alipe jeshi letu lote nguvu za kumuaibisha shetani kwa kushinda vita.
Hongera kwa KDF na AMISOM yetu. Tuko nyuma yenu. Endeleeni na kuwatokomeza wakatili hao.
Dada na kaka zetu wapondeni maadui hawa hadi roho ya mwisho. Ninawaungeni mkono sana. Hongera.
Wasomali msifanye tena makosa baada ya kukomboa nchi yenu kutokana na propaganda za magaidi chini ya kivuli cha dini. Kumbukeni sio mara ya kwanza nchi yenu kukombolewa toka mkononi mwa magaidi halafu wenyewe kuikabidhi tena kwa hao hao magaidi. Waethiopia waliwasaidia kuwaondoa magaidi halafu mkaambiwa hao ni makafir hawana sifa ya kuwasaidieni kuleta utulivu kwenye nchi yenu mkafanya 'jihad' mkairejesha nchi mikononi mwa magaidi kwa mara nyingine. Kumbukeni dini inamfaa mtu kwa binafsi yake kwenda mbinguni na kamwe haipaswi kuchanganywa na siasa. Hapa Ulimwenguni kinachohitajika ni 'reason and logic' Mkizingatia hilo hakika Somalia iliyokua na heshima tele itarejea.
Kazi nzuri, Mungu awabariki KDF, AMISOM na TFG. Tunaomba Mungu mrejee nyumbani nyote baada ya kumaliza kazi.
Kuweni wenyewe kwa vile mnaenda kuwatokomeza al-Shabaab watoke Kismayu na tunawafuateni kwa dua zetu.
Nyinyi ni wajumbe wa amani katika Afrika ya Mashariki. Sote tunawaombea. Nyinyi ndio washindi. Endeleeni.
Mungu awabariki askari wetu wa Kenya na askari wenzao kwa vile wanapigania amani ya Afrika. Mungu awabariki nyote kwa kwenda na kurejea kwenu. Amani, amani, amani, Amin...
JAMANI WATANZANIA ULAFI NA UBINAFSI WA VIONGOZI WA KADA ZOTE ZA UMMA NA SEREKALI KUU ZINATOKANA NA MTU MWENYEWE NA SI CHAMA .CHAMA KINACHOANGALIA UKABILA, UDINI HIVI HAVITUFAI KABISI NI KHERI TUKABAKIA HIVYO HIVYO KAMA TULIVYO ACHWA NA MWALIMU NYERERE KULIKO KUKIPA CHAMA KINACHAO ANGALIA UKABILA NA UDINI KUSHIKA HATAMU.INCHI YETU UKIANGALIA SYSTEM ILIYOACHWA NA MWALIMU ,VIUONGOZI WA NGAZI ZA JUU WANATOKA KATIKA JAMII YA KWAWAIDA SANA KULIKO HAYA YANAYOTOKEA KWA CHAMA HIKI KINACHOKUJA KWA KASI YAANI CHADEMA .HIKI CHAMA KIINA UKABILA NA UDINI NA UKIANGALIA SOURSE YA CHAMA HIKI KIMETOKE KWENYE UZAO WA KINA MANGI SINA.nI VIZURI VIONGOZI WACHACHE WENYE KUJILIMBIKIZIA MALI WAKACHUKULIA HATUA KULIKO KUNGOA MTI ULIOTA KWENYE JANGWA WAKATI MATUZO YAKE TULIYAKUZA KWA SHIDA SINA CHAMA ILA NI MWONO WANGU. wATANZANIA TUWE MAKINI .........
Bwana Mungu wetu awe pamoja nanyi ili kuwasafisha al-Shabaab moja kwa moja. Sote tumo kwa maombi.
KAZI NZURI KDF, AMISOM. ENDELEENI NA MOYO WA KUPAMBANA ILI KUWEPO NA AMANI NCHINI KWETU NA JIRANI YETU SOMALIA. WAKENYA TUOMBE KWA WATOTO HAWA WANAOPIGANA NA MAGAIDI HAWA. JOSEPH SHIKUKU MUNG'ALA-ELDORET
Eee Mungu kumbuka familia, wanawake na watoto waepushe na vifo.Yeyote anayetaka kuona kile kinachoendelea au kile mnachofanya, watakeni wawe wavumilivu. Kwa hali yoyote ile, walikuweko wapi wakati al-Shabaab ilikuwa ikiwachinja watu. Mashirika ya kiraia hawafai kutoa maoni Tuwasaidie pale inapowezekana lakini tusilaani kazi nzuri ya AMISOM na KDF asanteni kwa kazi yenu. Endeleeni . Mwenyezi Mungu awe pamoja nanyi katika hali zote.
Mungu awe pamoja nanyi vijana (KDF) waukamate mji huo na warejee nyumbani!!! Hongera!!
Wapendwa askari wetu kuweni na ujasiri wa kuwashinda hao al-Shabaab. Na mimi hapa ninaomba kwa Mungu awalinde na afanye ngao kupitia damu yake na mtaibuka washindi . Hongera.
Itakuwa habari nzuri ikiwa Kismayo itaanguka kwa AMISOM.
Al-Shabaab wanaoishi kwa upanga waachwe wafe kwa upanga, mafundisho ya Biblia yanaonesha hivyo.
Mungu wabariki wanawake na wanaume wa KDF kwa vile wanapambana kufanikisha kazi hii ya heshima.
Tuwaombeeni Luteni Shukri Mohamed Abdi na wenzake wa KDF na TFG: na wale wote wanaojali kuhusu Somalia. Mwenyezi Mungu awalinde vijana wetu wa ulinzi katika kuelekea kwao Kismayo na hata Mogadishu. Amin, amin, amin, Ewe mwenyezi Mungu.
Tabaka la watu wa juu kutoka Somalia wanaoishi Kenya lazima wachangie katika mchakato wa amani kwa kuisaidia Kenya kuwatambua wahalifu wanaowalenga watu wetu katika kambi ya wakimbizi ya Dadaab na sehemu nyengine za nchi.
ni makala nzuri
Endeleeni AMISOM, iliyo kuu na imara, ninawaombeeni dua kutoka alfajiri hadi jua kutua.
Kazi nzuri, Mungu akusaidieni.
Vidole vya gumba juu kwa KDF na AMISOM. Ni wakati kwa nguvu za giza nchini Somalia kusagwa mpaka kusalimu amri. Mungu Ibariki Kenya, Mungu Ibariki Somalia, Mungu Ibariki Afrika. Al-Shabaab ipotelee mbali. KDF na AMISOM tumesimama pamoja na nyniyi na Mungu awape ushindi.
KDF tuko nyuma yenu, endeleeni.
Kwa kuwa kazi nzuri inatendeka katika operesheni hii, tuwashukuru na kuwapa moyo na ari KDF wetu pamoja na askari wa AMISOM ambao wamejitolea kuilinda nchi yetu (Kenya). Hata hivyo, ninasumbuliwa na kituo cha habari kinachoendelea kutangaza, mipango ya AMISOM na KDF pamoja na maendeleo yaliyofikiwa. Ndio! Wanatujuza habari moto moto, lakini wawe na tahadhari habari hizi zisitumiwe na al-Shabaab kujipangia mikakati au kuifanya mipango hii kuwa migumu. Tafadhali, tafadhali, tafadhali” Bwana (majina yako yote yanazingatiwa) msemaji, simamia habari inayotumwa kwa watu wa habari, wawe wa kitaifa, kikanda au wa kimataifa. Ikiwa inawezekana, toeni habari baada ya mashambulizi kwishafanyika. Yeyote anayetaka kuona kile kinachoendelea au kile mnachofanya, watakeni wawe wavumilivu. Kwa hali yoyote ile, walikuweko wapi wakati al-Shabaab ilikuwa ikiwachinja watu. Mashirika ya kiraia hawafai kutoa maoni zao za kipuuzi. Tuwasaidie pale inapowezekana lakini tusilaani kazi nzuri ya AMISOM na KDF. Vyenginevyo, KDF na AMISOM, asanteni kwa kazi yenu. Endeleeni vijana, wanawake na wanaume. Mwenyezi Mungu awe pamoja nanyi katika hali zote.
Aha! Acha nisubiri matokeo. Mnaunga mkono uvamizi shaghalabaghala na usiopangwa nchini Somalia ambapo wageni ni chakula moto. Kismayo si pahali maalumu kwa KDF, askari wa kukodiwa wa Museveni na Burundi ambao ni watafuta maisha. Baada ya Kismayo tuhesabu upotevu wa wachokozi hawa.
Vikundi vya KDF na AMISOM, kazi nzuri! Ukombozi kamili unakuja kwa Somalia na nchi Jirani. Mko mioyoni mwetu na tunawaombea. Hatimaye mtashinda vita hivi. Mungu yuko nyuma ya juhudi zenu kwa vile mnapigania amani. Awajaalieni Ushindi wote. Momanyi.
Hawa al-Shabaab ni mbwa wa ngono. Ni lazima waishi kwa kulamba vidonda vya waliokufa. Hakuna kurudi nyuma kwa TFG na AMISOM. Watawakomboa Wasomali ambao ni watu wema ili wafaidi matunda ya nchi yao. Operesheni Linda Nchi inaendelea. Wapigeni maadui wa watu wa Somalia. Wasafisheni katika choo.
Kwa nafsi yangu, nimefurahia sana na mwendeleo ambao AMISOM imefika mpaka leo. Mungu aliye na nguvu awe na jeshi letu katika wakati huu mgumu.
Vikosi vya KDF, TFG na AMISOM mpo katika nafasi nzuri ya kuiteka Kismayo kwa usiku mmoja na nadhani mmeshapitiliza muda zamani. Ikiwa naweza kuuliza, kwa nini mnawaacha viongozi wa al-Shabaab kukimbia kutoka Kismayo? Pili, bado mnashawishika kuwa viongozi wa kikundi hiki hawaishi Kenya na kufanya shughuli zao pamoja na viongozi wetu? Kwa nini sisi (wananchi wa kawaida) tuendelee kuteseka mikononi mwa al-Shabaab wakati “viongozi wetu" wanafaidi pesa za uharamia. Ili kuwapa al-Shabaab pigo la mwisho, vita vingeanzia na Eastleigh – Nairobi kabla ya kupelekwa Somalia.
Kurejeshwa kwa uhuru wa fikira kupo karibu. Shikilieni hapo hapo.
Kazi nzuri jeshi letu. Endeleeni.
Al-Shabaab inaishi zama za kale na wanahitaji kusasisha itikadi yao
Ninaunga mkono operesheni hii kwa vile ni vyema kuwa na serikali kwa ajili ya watu wa Somalia. Hili litawasaidia kuiendeleza nchi yao na kuwa na uhuru wa kuishi kwa mtindo wa maisha yao wenyewe.
Endeleeni na kazi nzuri, waacheni watu wa Somalia wafurahie uhuru, daima tunamuomba Mungu awape watu wa Somalia amani na waweze kuendeleza nchi yao.
Nimefurahi kwa venye KDF ilichukua muda kuwashambulia al-Shabaab huko Kismayo, kwa sababu wanamgambo wamewashikilia raia kwa usalama wao wenyewe kama ngao yao. Walitaka kujificha wenyewe kwa haki za binadamu za UN, kwamba KDF imewaua raia, lakini sasa hawatawalaumu KDF, watawalaumu AMISOM na hawa wanalindwa na UN. Jeshi la Ulinzi la Kenya limepewa mafunzo mazuri na litawashughulikia al-Shabaab bila huruma. Watajuta kuishambulia Kenya. Upelelezi wa Jeshi la Ulinzi la Kenya imekamilika, kwa sasa al-Shabaab wako kimya kwa vile hawaelewi mpango wa Kenya.
Nadhani hili ni jaribio la kukusudia ili kudharau juhudi za KDF. Maoni yangu ni kuwa hii sio haki, AMISOM ni nini, walikuwa wapi wakati KDF walipoleta amani maeneo makubwa yaliyokuwa yanakaliwa na al-Shabaab? Kwa vyovyote vile, enyi mashujaa wa KDF, endeleeni na kazi nzuri. Hongera
Mubarikiwe kwa kazi ya mikono yenu na mpewe nguvu za kuwashinda watu hao mpaka mwisho.
Al-Shabaab imewaua watu wa Kisomali na yanayofanyika hayawezwi kufanywa na mtu Msomali, lakini ni matokeo ya itikadi ya unyama ambayo imejificha chini ya mambo ya dini. Watu wa Kisomali watakuwa imara na kupumzika siku moja bila ya kujali shida ambazo wanapitia kama mauaji, wizi na uporaji wa mali zao na vikundi hivi. Vikosi vya serikali isishambulie maeneo ambayo wengi wanoishi ni raia kwa sababu hii italeta vifo vya watu zaidi hii ikifanyika. Serikali lazima iwe na hadhari ya hali ya wananchi wake.
AMISOM wawe na tahadhari wasiwadhuru wananchi wasio na hatia. Ni hatua nzuri, endeleeni.
Hiyo ni kweli meja...Bila ya KDF operesheni haitafanikiwa.
Ninajivunia na kile kinachoendelea Somalia mpaka sasa. Kinachohitajika sasa ni mpango mzuri na taratibu za mkabala wa kimbinu. Ni suala la wakati tu, Kismayo itakuwa katika ukanda unaomilikiwa na jeshi. Ndio, kunaweza kutokea vifo huko. Kitu muhimu ni kuusafisha mji wote na wananchi wafurahie kuliko wakati waliokuwa wametekwa nyara na al-Shabaab. Chukueni wakati, lakini lazima mshinde vita hivi. Mbele daima, nyuma mwiko. HONGERA, sisi tunawaangalieni na tunawaoombeeni dua nyinyi na Somalia siku moja itafurahia AMANI - Mlinda Amani wa Zamani, Timor ya Mashariki Mstaafu C.I. Noah Tanui.
Ni makala nzuri, sio sahihi kumuua kijana ambaye bado hajaoa hadi kufa hata kama amefanya tendo la zinaa, hii ni kwa mujibu wa Koran Tukufu
Hii ni hadithi ya watu walio katika hali ya ulevi. Mtu huyu anayepigwa huko Qoqani na Kolbiyo na kudang'anya umma afanye anavyoweza...Kuiweka nchi chini ya utawala wa watu waliofunikwa ni bora kuliko kuiweka chini ya utawala wa kikoloni wa Afrika.
Ingawa nimefurahishwa na habari nzuri ya maendeleo ya mpango wa TFG kuikamata Kismayo, na kama kuna sababu nzuri ya kutotaja nani aneyehusika na maendeleo haya, nadhani ni makosa kutoitaja KDF ambayo imechukua uongozi wa kuikamata Kismayo kutokana na ukweli kwamba wana nguvu ya kuwatoa al-Shabaab Kismayo na kuwakomboa watu wa Somalia. Meja (Mstaafu) Sila Mutungi.
Amani iwe juu yenu. Tunamuomba Mungu kuwafanya al-Shabaab wamezwe na ardhi.