Mashindano ya mpira wa kikapu yamalizika Hargeisa

Na Barkhad Dahir, Hargeisa

Juni 13, 2012

  • 4 Maoni
  • Chapisha
  • Panga upya Punguza Ongeza

Timu ya Abaarso Tech iliishinda Prison Corps kwa vikapu 36-25 katika mchezo wa mwisho wa mashindano ya mpira wa kikapu ya wiki mbili ambayo yalimalizika Jumatatu (tarehe 11 Juni) huko Somaliland.

  • Vijana wa timu ya Abaarso Tech wakisherehekea ushindi wao dhidi ya timu ya Prison Corps, kwa kupata ushindi katika mashindano ya mpira wa kikapu huko Hargeisa. [Barkhad Dahir/Sabahi]

    Vijana wa timu ya Abaarso Tech wakisherehekea ushindi wao dhidi ya timu ya Prison Corps, kwa kupata ushindi katika mashindano ya mpira wa kikapu huko Hargeisa. [Barkhad Dahir/Sabahi]

  • Timu ya Abaarso Tech (wekundu) na Prison Corps (weusi) wakicheza mpira wa kikapu katika Uwanja wa Timo Adde huko Hargeisa. [Barkhad Dahir/Sabahi]

    Timu ya Abaarso Tech (wekundu) na Prison Corps (weusi) wakicheza mpira wa kikapu katika Uwanja wa Timo Adde huko Hargeisa. [Barkhad Dahir/Sabahi]

Mashindano hayo yaliandaliwa na Wizara ya Vijana, Michezo na Utamaduni na Shirikisho la Mpira wa Kikapu Somaliland, na kudhaminiwa na Mercy Corps kwa ushirikiano na Shirika la Kimataifa la Marekani kwa ajili ya Maendeleo (USAID).

Waziri wa Vijana, Michezo na Utamaduni wa Somaliland Ali Said Raygal alisema mashindano hayo yalikuwa sehemu ya juhudi za wizara za kuimarisha michezo Somaliland na kusaidia kujenga uwezo wa vijana kimwili na kiakili.

Mashindano hayo yalikuwa ya kwanza ya aina yake Somaliland tangu serikali kuu ya Somalia kuanguka miongo miwili iliyopita, kwa mujibu wa mkurugenzi wa Shirikisho la Mpira wa Kikapu Somaliland, Mohamed Abdullahi Qodah.

Alisema mashindano hayo yalikuwa na “umuhimu mkubwa kwa sekta ya michezo ya Somaliland”.

Timu sita zilishiriki mashindano katika Uwanja wa Timo Adde: Abaarso Tech, Prison Corps, SOHASCO (shirika la ndani lisilo la kiserikali), Chuo Kikuu cha Alpha na timu mbili zilizowakilisha vijiji vya Mohammad Moge na Jigjiga-yar huko Hargeisa.

“Lengo la mashindano ilikuwa ni kuwahamasisha vijana kushiriki katika michezo kwa sababu kujumuika ni muhimu kwa kukuza kiwango cha michezo [katika jamii],” Qoodah alisema. “ Tutajaribu tuwezavyo ili kuwahamasisha vijana kushiriki katika michezo ili kuwaepusha na kujihusisha na vitendo vya kigaidi na matumizi ya madawa, vitu ambavyo ni tatizo kwa Somaliland.”

Sherehe za ufungaji zilihudhuriwa na Waziri wa Vijana, Michezo na Utamaduni, Kamishna wa Magereza Mohamed Hussein Farah, Katibu Mkuu wa Wizara ya habari ya Somaliland Mohamed Hussein Farah, Mkurugenzi Mkuu wa Waziri wa Vijana, Michezo na Utamaduni Mustafe Mohamed, na mkurugenzi wa Shirikisho la Mpira wa Kikapu la Somaliland na mashabiki wa mpira wa kikapu.

“Katika mashindano yoyote, moja ya timu mbili hushinda, na huifanya timu iliyoshindwa kujaribu zaidi ili kushinda katika mashindano yajayo,” Raygal alisema katika hotuba yake wakati wa maadhimisho ya ufungaji.

Naye kamanda wa timu ya Prison Corps aliipongeza timu ya Abaarso Tech kwa ushindi. “Tutajaribu kadri tuwezavyo kushinda katika mashindano ya mwaka ujao na nitaimarisha timu yangu,” Farah alisema.

Raygal alikabidhi kombe la ushindi kwa timu ya Abaarso Tech na kuwapongeza. Pia alikabidhi sare za michezo kwa wachezaji wawili, mchezaji aliyeshinda vikapu vingi wakati wa mashindano na mchezaji bora katika mashindano.

Raygal alisema wizara inapanga kujenga viwanja zaidi vya michezo ili kuwapa vijana fursa ya kushiriki katika aina tofauti za michezo na kuwahamasisha wapende michezo zaidi.

“Ninapenda kuyaomba makampuni binafsi na mashirika ya ndani na ya kimataifa kutusaidia kutekeleza mipango hii,” alisema.

Unaonaje kuhusu makala hii? (Jumla ya Kura 10)

Dislike_icon(0)

(Sera za kutoa Maoni) *Inaonesha Maeneo yanayohitaji

Maoni ya msomaji

  • mustafe
    July 6, 2012 @ 04:43:29AM

    Ninaipongeza timu ya Abaarso kwa kushinda kombe.

  • siciid bodhle
    June 17, 2012 @ 10:03:35AM

    Nimefurahi kweli kwa Abaarso kushinda kombe na wakati huo huo kuwataka waendelee na moyo huo huo.

  • Hussein Egal
    June 15, 2012 @ 01:40:23PM

    Ningependa kuipongeza timu ya Abaarso Tech ambayo ilishinda mashindano hayo. Kwa kweli wamefanya vizuri sana. Naamini kuwa haya ni maendeleo mazuri ambayo yanawapatia fursa vijana kuondokana na kujihusisha na utumiaji wa dawa za kulevya na dhidi ya wale wanaowapa sumu ya itikadi za kupotosha.

  • Yusur
    June 14, 2012 @ 02:14:51AM

    Inahamasisha kusikia habari kuwa vijana wa Somalia mnajishughulisha na michezo ili kujiepusha na uovu wa kutumia madawa ya kulevya au shughuli za KIHALIFU.

Habari Mpya kabisa

Katika Mwangaza

Jisajili

Kura

Je, unadhania kupigwa marufuku kwa hotuba ya chuki na Tanzania kutakomesha mashambulizi dhidi ya makanisa na misikiti?

Angalia matokeo