2013-05-24 Mkutano wa Ujenzi Mpya wa Somalia, Uwekezaji na Maonesho mjini Nairobi -- uliopangwa tarehe 28 hadi 29 -- utawahamasisha wawekezaji kusaidia kuijenga upya Somalia.
2013-05-24 Kiongozi wa ngazi ya juu wa al-Shabaab Ahmed Abdi Godane anajaribu kupotosha mfululizo wa ukosoaji unaomlenga yeye kutoka kwa viongozi wengine waandamizi kwa kuwaita 'majahili' na "waovu'.
2013-05-23 Baada ya waandamanaji kubomoa daraja, kuchoma nyumba na ofisi za chama tawala mjini Mtwara, Waziri wa Mambo ya Ndani Emmanuel Nchimbi aliliambia bunge kwamba lazima hatua zichukuliwe.
2013-05-23 Uhusiano wa kidiplomasia baina ya nchi hizi mbili umekanganyika kufuatia kuhukumiwa kwa Wairani wawili walioshukiwa kupanga shambulizi la kigaidi nchini Kenya.
2013-05-22 Huku kukiwa na ongezeko la usajili katika vyuo vikuu, Shirikisho la Waajiri Kenya na wengine wanauliza iwapo wahitimu wanapata mafunzo yanayofaa kwa ajili ya kazi.
2013-05-22 Katika mahojiano ya kina na Sabahi, Msemaji wa Misheni ya Afrika Mashariki nchini Somalia Kanali Ali Aden Humad alizungumzia kuhusu jinsi AMISOM wanavyowasaidia Wasomali kuleta amani na utulivu.
2013-05-21 Serikali inafanyakazi ya kusafisha barabara zinazounganisha Mogadishu na Marka na Baidoa ili wananchi waweze kusafiri bila ya kuzuiwa na wanachama wanamgambo.
2013-05-21 Kutokana na vurugu za kuvuka mipaka, Kaunti ya Mandera inatafuta ushirikiano kutoka kwa maafisa na viongozi wa jamii mbalimbali huko Kenya, Ethiopia na Somalia.
2013-05-20 Kupitia ushindani mpya, kampuni ya mawasiliano ya simu inawahamasisha vijana wa Kenya kuandaa programu za simu ya mkononi ambayo yanaweza kuwaleta fedha na kuleta matokeo mazuri kwa nchi.
2013-05-20 Tanzania inafanya jitihada za kupambana na rushwa lakini viongozi wanahitaji mamlaka zaidi ili kuliondosha kabisa, mkurugenzi mkuu wa taasisi ya kuzuia rushwa Edward Hoseah aliiambia Sabahi.
2013-05-17 Ingawaje polisi wameshawakamata na kuwahoji zaidi wa watu 300 kuhusiana na mashambulizi hayo, uchunguzi bado haujagundua sababu.
2013-05-17 Vikundi vya vyama vya kiraia vinakusanya saini kwa ajili ya kuwafuta kazi wabunge saba kwa kujaribu kubadilisha makato ya mishahara kwa maofisa wa umma.
2013-05-16 Serikali ya shirikisho ilitangaza kwamba itachukua udhibiti kamili wa eneo la anga lake ifikapo mwishoni mwa 2013, harakati ambazo zimesababisha utawala wa Somaliland kuchukua hatua kinzani.
2013-05-16 Viongozi wawili kutoka koo pinzani wanadai nafasi ya juu katika jimbo la kusini ya Somalia linalogombaniwa, huku serikali ya shirikisho ikifikiria kuingilia kati na kuwapatanisha.
2013-05-15 Wakosoaji wasema Kenya haijafanya vya kutosha kubainisha rushwa inayofanywa na polisi, wakati maofisa wa polisi wanasema fedha zaidi zinahitajika kupanga polisi pamoja na kuondoa mfumo wa serikali.
2013-05-15 Vyama vikuu viwili vya wafanyakazi nchini, Chama Kikuu cha Wafanyakazi wa Djibouti na Umoja wa Wafanyakazi wa Djibouti, vinapaswa kuunganisha nguvu zao ili kutetea haki za sehemu za kazi, wafanyakazi wasema.
2013-05-14 Serikali ya Somalia inajaribu kuanzisha ujumbe mpya wa kidiplomasia duniani kote ili kuonesha sera zake juu ya uchumi na maendeleo ya binadamu.
2013-05-14 Viwango vya elimu vyenye uwiano vingeweza kutoa fursa kwa raia na makampuni katika Jumuiya ya Afrika Mashariki kuvuka mipaka kutafuta ajira na fursa, wadau wasema.
2013-05-13 Zaidi ya wanawake 200 wa Somalia wasiojua kusoma, kuandika wala kuhesabu wanapata mafunzo ya bure katika shule ya Wilaya ya Waberi.
2013-05-13 Kama sehemu ya jitihada za kuondoa kabisa vitisho vya al-Shabaab, serikali inafufua askari wa akiba wa Kenya, kikosi cha raia wenye silaha ambao wataingia kama askari kanzu katika jamii zao.
2013-05-10 Kituo cha Operesheni za Polisi Kenya kitaipa nchi makali ya kuzuia vitisho vya wenye msimamo mkali kwa kuratibu juhudi za pamoja baina ya idara za usalama, maafisa wa serikali wasema.
2013-05-10 Washiriki wa mkutano waliahidi takribani dola milioni 450 kama msaada kusaidia serikali ya Somalia kujenga tena nchi na vikosi vyake vya jeshi.
2013-05-09 Suala lenye utata juu ya haki ya kuchinja wanyama pia lilishughulikiwa katika mkutano huo, na viongozi wa dini wanapanga kutoa kanuni mpya kwa vyombo vya habari karibuni.
2013-05-09 Ahmed Abdi Godane alirudia maudhui yake ya kawaida bado akishindwa kushughulikia ukosoaji anaokabiliwa nao kutoka kwa viongozi kadhaa wengine wanaoongezeka wa ngazi ya juu wa al-Shabaab.
2013-05-08 Wakaazi na maofisa wa ndani wasema mafuriko yamesababisha hali ya kukata tamaa ambayo inaweza kuongeza migogoro ya kibinadamu ambayo inahusisha kuenea kwa njaa na magonjwa iwapo msaada hautapatikana.
2013-05-08 Raychelle Awuor Omamo, mwanadiplomasia wa muda mrefu na mwanasheria, ni mteule wa baraza la mawaziri la Raisi Uhuru Kenyatta kwa nafasi ya waziri wa ulinzi.
2013-05-07 Raia wanazisaidia mamlaka kuulinda mji dhidi ya ugaidi kwa kuripoti matukio yasiyo ya kawaida na vifurushi visivyo wenyewe.
2013-05-07 Mlipuko huo uliwaua watu watatu na kujeruhi zaidi ya 60, huku serikali ikiapa kutumia 'nguvu za hali ya juu' kupambana na wale wanaojaribu kuchochea mvutano wa kidini nchini.
2013-05-06 Rais Jakaya Kikwete ametoa amri kwa vikosi kupambana na majangili moja kwa moja, wakati Mbuga za Wanyama za Tanzania zimetangaza mpango wa kutumia ndege za uchunguzi zisizokuwa na marubani.
2013-05-06 Waziri huyo aliiambia Sabahi kwamba jamii ya kimataifa lazima iendelee kusimama na Somalia ili kujenga juu ya maendeleo yaliyopatikana hadi sasa na kutambua nguvu zake kamili za kiuchumi.
2013-05-03 Mpango mpya unakusudia kumaliza suala la kutokuwa na makazi na kuwapeleka watoto wadogo shule na kutoa elimu ya amali kwa vijana.
2013-05-03 Mmoja wa anayeshukiwa kuwa kati ya washambuliaji wa shambulio la mwezi uliopita kwenye ofisi ya gazeti la Hubaal ni ofisa wa polisi, ukweli ambao unasababisha wengi kuamini kwamba maofisa wa serikali wanahusika.
2013-05-02 Wizara ya Mambo ya Ndani na Usalama wa Taifa ya Somalia hivi karibuni kitahamasisha kitengo cha polisi 1,300 kufanya doria katika mji mkuu wa nchi wakitumia gari na helikopta zilizowekwa alama maalumu.
2013-05-02 Kenya imefanya maendeleo kidogo katika utekelezaji wa dira yake ya 2030 ya mpango wa maendeleo, wakosoaji wasema, lakini maofisa wanaoisimamia wasema nchi inapata maendeleo ya kuridhisha.
2013-05-01 Mwezi ujao, wafanyabiashara wengi watatakiwa kuanza kutoa risiti zinazosajili kodi kielektroniki ili kuhakikisha kwamba serikali inakuwa na kumbukumbu sahihi za mauzo yao.
2013-05-01 Serikali ya shirikisho ni lazima iwekeze katika uanzishaji upya na kurekebisha matatizo ya kiuchumi ili kuweka uchumi wa Somalia katika njia inayoelekea kwenye ukuaji endelevu.
Zaidi ya wanawake 200 wa Somalia wasiojua kusoma, kuandika wala kuhesabu wanapata mafunzo ya bure katika shule ya Wilaya ya Waberi.
Timu za mpira wa miguu za Al-Badar na Badbaado zikijipanga kwa ajili ya mechi ya Kundi B la Ligi ya Taifa ya Somalia kwenye Uwanja wa Chuo Kikuu cha Taifa hapo tarehe 29 Aprili, 2013. Washabiki wengi walijitokeza kushangilia timu hizo mbili na kufurahia mechi, shughuli ambayo hapo mwanzo ilipigwa marufuku na al-Shabaab wakati wanamgambo walipokuwa wanaudhibiti mji mkuu.